Habari za Punde

WAZIRI YA AFYA ZANZIBAR YAPOKEA MSAADA KUTOKA WHO

Muakilishi wa Shirika la la Afya duniani WHO Ghirmay Andemichael  wapili kutoka kushoto akitoa maelekezo ya  vifaa mbali mbali vilivyotolewa msaada kwa Wizara ya Afya huko Mnazimmoja Zanzibar. 

Muakilishi wa Shirika la la Afya duniani WHO Ghirmay Andemichael akimkabidhi mashine ya kupumilia Mkurugenzi Mkuu Wizara Afya Dk Jamala Adam Taib ikiwa ni miongoni mwa vifaa vilivyotolewa msaada kutoka kwa WHO kwenda Wizara ya Afya Zanzibar huko Ofisi ya  Wizara ya Afya Zanzibar. 

Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar  23/10/2020

WAZIRI wa Afya Zanzibar Hamad Rashid Mohamed amelitaka  Baraza la Wataalam wa Maabara ya Tiba kusimamia maadili  ili kuhakikisha huduma zinazotolewa katika maabara au taasisi nyengine zina ubora unaokubalika 

 

Akiyasema hayo katika Uzinduzi wa Baraza la wataalam wa Maabara ya Tiba Zanzibar katika ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazimmoja.

 

Alisema kusimamia maadili kwa wafanyakazi kutasaidia kutekeleza majukumu ya watendaji ili kukidhi kiwango bora cha utekelezaji

 

Waziri huyo alisema Baraza la Wawakilishi Zanzibar  lilipitisha na kuidhinisha sheria nambari 10 ya Wataalam wa Maabara za Tiba  Zanzibar mnamo Mei 11, 2020 .

 

Alifahamisha kuwa chombo hicho kina majukumu ya kutambua wataalamu sahihi wa maabara za Tiba na kusimamia haki zao .

 

“Wataalamu wawe na kiwango cha ujuzi kutokana na kuwa wanashughulikia maisha ya watu” alisema Waziri Hamad.

 

Alieleza sambamba na majukumu hayo pia chombo kimepewa uwezo wa kuwajibisha watendaji pale ambapo watakapo kwenda  kinyume na sheria iliyopo.

 

Aidha alisema huduma za maabara ni moja kati ya huduma za uchunguzi wa maradhi mbali mbali unaofanyika Maabara (laboratories)  kwa kutumia sampuli za kila aina zinazopatikana kutoka kwa binaadamu ambazo huduma hizo hutolewa katika Hospitali za Serikali  na za binafsi.

 

Waziri Hamad alisema kuwepo kwa sheria ya wataalam wa maabara za tiba Zanzibar itasaidia wataalam hao kusajiliwa  hapa Zanzibar baada ya Tanzania bara na pia kudhibiti watu wasiostahiki kupima vipimo vya maabara na kutoa majibu yasio sahihi ambayo huhatarisha matibabu na usalama wa wagonjwa.

 

Nae Mwenyekiti wa Baraza la Wataalamu wa Maabara za Tiba Zanzibar Dkt Salum Seif Salum alisema jukumu la baraza hilo ni kuhakikisha wanatoa leseni na vyeti na kufuatilia taarifa zozote zinazohusiana na usajili pamoja na kubadilisha cheti na leseni iiliyothibitika kuibiwa au kupotea.

 

Pia alisema kusimamia viwango vya utendaji wa wataalamu wa Maabara ya Tiba na kuhakikisha  umahiri wa Wataalamu wa Baraza za Tiba .

 

Alieleza kuwa Baraza lina jukumu la kushughulikia malalamiko yaliyowasilishwa dhidi ya Wataalamu wa Mabaraza ya tiba na kumshauri Waziri juu ya mambo yanayohusiana na utoaji huduma .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.