Habari za Punde

Matumizi mabaya ya Rasilimali hupelekea kuwepo migogoro ya kijamii


Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia  Dkt. Salim Hamad alipokuwa akiwasilisha Mada katika mafunzi elekezi kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Chukwani.


na Mwandishi wetu
 

Mhadhiri wa Chuo cha Diplomasia  Dkt. Salim Hamad amesema matumizi mabaya ya rasilimali za asili ikiwemo  gesi na mafuta ni miongoni mwa sababu zinazopelekea kuwepo kwa migogoro ya kijamii.

 

Dkt. Salim amesema hayo wakati akiwasilisha mada inayohusiana na maliasili na vyanzo vya migogoro ya kijamii katika mafunzo elekezi kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi huko Chukwani.

 

Amesema  jamii kadhaa ulimwenguni zinakabiliwa na migogoro mingi inayosababishwa na matumizi mabaya ya rasilimali hizo, hivyo  amewasisitiza  Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kusimamia vyema Sekta hii kwa kutunga Sheria,Kanuni na miongozo bora na hatimae rasilimali ya mafuta na gesi asilia  kuweza kuchimbwa kwa maslahi ya taifa zima.

 

Amewataka wajumbe hao kuangalia maeneo yote yanayoweza kuleta changamoto na kuibua migogoro katika upatikanaji wa rasilimali ya mafuta na gesi na kuyaainisha ili yaweze kupatiwa ufumbuzi mapema kabla ya utumiaji wa rasilimali hizo.

 

Nao wa jumbe wa BLW kwa upande wao wameishukuru taasisi ya ZPRA kwa kuandaa mafunzo hayo yatakayosaidia kutoa uelewa katika muktadha wa kufahamu vyanzo halisi vya migogoro na namna bora ya kuitatua hasa migogoro itokanayo na rasilimali za asili.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.