RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemuapisha Suleiman Ahmed Saleh kuwa Katibu
wa Rais wa Zanzibar.
Hafla hiyo ya kiapo imefanyika leo Ikulu Jijiji Zanzibar.
Rais Dk. Mwinyi amemuapisha Katibu huyo baada ya
kumteua Novemba 4, mwaka huu kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya
kifungu cha 53 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Katika hafla hiyo viongozi mbali mbali walihudhuria, akiwemo Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dk. Mwinyi Talib Haji, Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Hassan Khatib , Naibu Kadhi Mkuu Sheikh Hassan Othman Ngwali, Viongozi wa Vikosi vya SMZ pamoja na viongozi mbali mbali kutoka Idara na taasisi mbali mbali za Serikali.
Kabla ya uteuzi huo Katibu huyo alikuwa Mkurugenzi Msaidizi katika Tume ya pamoja ya Fedha..
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment