Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi Azungumza na Uongozi wa Benki ya Standard Chartered Ikulu Jijini Zanzibar leo 18/11/2020.

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Bw.Sanjay Rughani alipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazunguzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu leo 18/11/2020 na kulia Mkuu wa Kitengo cha Masoko Bi. Juanita Mramba

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered Bw. Sanjay Rughani alipofika Ikulu Jijini Zanzibar na Ujumbe wake kuonana na kufanya mazungumzo (kulia) Mkuu wa Kitengo cha Masoko Bi. Juanita Mramba na Mkuu wa Kitengo cha Fedha Bi. Sapientia Balele.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiagana  na mgeni wake Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Benki ya Standard Chartered  Bw.Sanjay Rughani,  baada ya kumaliza mazungumzo yao  yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 18/11/2020


Rais Dk. Hussein  Mwinyi alikutana na uongozi wa Benki ya Standard Chartered ukiongozwa na Bwana Sanjay Rughani ambapo katika maelezo yake Rais Dk. Hussein aliueleza uongozi huo kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Awamu ya Nane imeahidi kufanya mambo mengi kwa wananchi hasa kwa kushirikiana na Sekta binafsi.

Alisema kwamba  Serikali iko tayari kushirikiana na  Taasisi mbali mbali zimkiwemo za binafsi  huku akisisitiza kwamba miongoni mwa taasisi hizo sekta ya benki ni muhimu sana.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Nane imeahidi mambo mengi kwa wananchi hivyo, mashirikiano na Benki ikiwemo Benki hiyo ya Kimataifa ya ‘Standard Chartered’ ni muhimu katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo.

Alieleza kwamba iwapo ipo fursa ya kukaa pamoja na kujadili miradi ipi ya kutekelezwa kwa pamoja Serikali iko tayari hasa ikizingatiwa kwamba Zanzibar inahitaji wawekezaji kuja kuekeza katika maeneo mbali mbali.

Nae kiongozi huyo wa ujumbe huo  Sanjay Rughani alimpongeza Rais Dk. Hussein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na kueleza matarajio yake makubwa kutokana na ari na hamu ya Rais huyo kuiletea maendeleo Zanzibar.

Kiongozi huyo alieleza kazi za Benki hiyo na namna inavyofanya kazi zake ndani nan je ya Tanzania huku akieleza azma ya Benki hiyo ya kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Sambamba na hayo, kiongozi huyo alieleza jinsi Benki hiyo inavyofanya kazi na Wizara ya Fedha na Mipango ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Wizara ya Fedha ya Zanzibar pamoja na Benki mbali mbali hapa nchini ikiwemo Benki Kuu (BOT).

Pamoja na hayo viongozi hao walieleza shughuli mbali mbali zinazofanywa na Benki hiyo katika kuisaidia jamii ikiwemo kutoa huduma za tiba ya macho, kuwasaidia watoto wa kike, uwekaji hakiba wa kifedha pamoja na mambo mengineyo.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.