Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Mhe.Dk Hussein Ali Mwinyi Azungumza na Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Kale na Utalii ya Oman.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Kale na Utalii kutoka Oman ukiongozi na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (kulia kwa Rais) Eng.Ibrahim Al Kharousy, Balozi Mdogo wa Oman  anayefanyia kazi zake Zanzibar.Mhe.Mohamed Ibrahim Al Balush na Bw.Ahmed Al Shekail Mhandishi wa Majengo Oman, wakifuatilia mazungumzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 15/12/2020
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe Lela Mohamed Mussa  akizungumza wakati wa mkutano na Ujumbe wa  Wizara ya Mambo ya Kale na Utalii kutoka Oman ukiongozi na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (kulia kwa Rais) Eng.Ibrahim Al Kharousy, Balozi Mdogo wa Oman  anayefanyia kazi zake Zanzibar.Mhe.Mohamed Ibrahim Al Balush na Bw.Ahmed Al Shekail Mhandishi wa Majengo Oman, wakifuatilia mazungumzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar 
 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi alikutana na ujumbe kutoka nchini Oman na kubadilishana nao mawazo juu ya maendeleo ya kulifanyia matengenzo makubwa jengo la Beit el Ajaib liliopo Forodhani Jijini hapa pamoja na changamoto zilizojitokeza.

Dk. Mwinyi aliipongeza serikali ya Oman kwa juhudi kubwa inazozichukuwa katika kulifanyia matengenezo jengo hilo, kwa mujibu wa mkataba wa makubaliano (MOU).

Amesema hatua ya kulifanyia matengenezo jengo hilo itasaidia kulirejeshea  katika hali yake ya asili, na hivyo kuendelea kutumika na kuimarisha Utalii.

Aliishukuru Serikali ya Oman kwa msaada wake na hivyo kumuomba kiongozi wa ujumbe huo kumfikishia salamu za  kheri kiongozi wa Taifa hilo.

Nae, Waziri wa Mambo ya Kale wa Oman Ibrahim Al Kharous alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kufuatilia kwa karibu matengenezo ya jengo hilo muhimu katika ustawi wa sekta ya utalii nchini.

Mapema, Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale.Mhe. Leila Mohamed Mussa alisema jengo la Beit  al Ajaib ni muhimu sana katika maendeleo ya utalii nchini na kubainisha idadi kubwa ya wageni wanaolitembelea pale wanapozuru nchini.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 

 E-mail: abdya062@gmail.com


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.