Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) Justina Mashiba (kulia) akikabidhi taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Mfuko huo kwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile. Katikati aliyeshika vitabu hivyo ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, Dodoma.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (aliyeketi katikati) akifuatilia maelezo ya mjumbe wa bodi ya UCSAF (hayupo pichani). Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula na wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu wa UCSAF, Justina Mashiba, Dodoma.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (aliyeketi katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa menejimenti ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote baada ya kikao chake na wajumbe hao, Dodoma. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula na wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu wa taasisi hiyo, Justina Mashiba.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt.
Faustine Ndugulile (aliyeketi wa pili kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
Dkt. Zainab Chaula (wa pili kushoto), Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi (wa
kwanza kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa
Mawasiliano kwa Wote baada ya kikao chake na wajumbe hao, Dodoma
Na. Celina Mwakabwale, UCSAF
Mtendaji
Mkuu wa mfuko wa mawasiliano kwa wote (UCSAF), Justina Mashiba amesema mpaka
sasa zaidi ya wananchi millioni 12 waishio maeneo ya vijijini na yasiyo na
mvuto wa kibiashara pamoja na wale wa mipakani na kanda maalum wamefikiwa na
huduma mbalimbali za mawasiliano ikiwemo simu, runinga, radio pamoja na
mawasiliano ya posta.
Bi.
Mashiba ameyasema hayo wakati wa ziara ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia
ya Habari Dkt. Faustine Ndugulile aliyetembelea tasisisi hiyo na kufanya kikao
na wajumbe wa bodi, menejimenti pamoja na wafanyakazi. Katika ziara hiyo
aliambatana na Katibu Mkuu, Dkt. Zainab Chaula, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Jim Yohazi pamoja na baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo.
Dkt
Ndugulile ameipongeza UCSAF kwa kufikisha huduma za mawasiliano kwenye maeneo
mbalimbali nchini huku akiitaka kuwekeza zaidi katika teknolojia yenye gharama
nafuu ili kuyafikia kwa haraka maeneo ambayo bado hayajafikiwa na huduma za
mawasiliano. Hivi sasa UCSAF inatumia shilingi milioni 350 kujenga mnara mmoja wa
mawasiliano.
Ameongeza
kwa kusema kuwa, sekta ya Mawasiliano na Teknolojia ya habari inabadilika kwa
kasi hivyo ameitaka wizara kukamilisha uandwaaji wa sheria ya TEHAMA ili
kuendana na kasi ya mabadiliko hayo.
Akizungumza
na wajumbe wa bodi Dkt Ndugulile ameagiza kuwepo na utaratibu mzuri wa kufanya
kazi kwa ukaribu na kwa ushirikiano kati ya Mamlaka ya mawasiliano Tanzania
(TCRA) na UCSAF ili kuongeza kasi ya upelekaji wa huduma mbalimbali za mawasiliano
katika maeneo wanayoshirikiana.
Nae Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula
ameipongeza UCSAF huku akiitaka kuendelea kufikisha huduma za mawasiliano ili
kuendana na malengo ya kuanzishwa kwa wizara hiyo.
Hadi sasa mfuko wa mawasiliano kwa wote umefanikiwa kufikisha
huduma mbalimbali za mawasiliano ikiwa ni pamoja na kuwasha minara katika kata
633 zenye vijiji 2,320, kuunganisha mtandao wa intaneti na kutoa vifaa vya
TEHAMA kwa shule 711, kutoa mafunzo ya TEHAMA kwa walimu 2,213 wa shule za UMMA
kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara pamoja na kujenga vituo 10 vya TEHAMA
visiwani Zanzibar.
Mfuko wa Mawasiliano Kwa Wote (UCSAF)
No comments:
Post a Comment