Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi Amefanya Matembezi ya Kugagua Mradi wa ZUSP Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa katika matembezi ya ziara yake kutembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa Huduma za Jamii Mjini Zanzibar (ZUSP) aliazia katika eneo la  barabara ya Kiembesamaki Uwanja wa Ndege kutembea na kujionea utekelezaji huo na kumalizia matembezi hayo katika eneo la mnazi mmoja na kuzungumza na Uongozi  unaosimamia Mradi huo, na (kulia kwa Rais) Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud Ali Mohamed na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo wakati akiwa katika matembezi ya kukagua maendeleo ya Mradi wa Huduma za Jamii Mjini Zanzibar (ZUSP) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrisa Mustafa Kitwana, wakiwa katika ziara hiyo kutembelea mradi huo wakipita katika eneo la Kilimani na (kushoto) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo na kutowa maagizo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa (ZUSP) akiwa katika eneo la kilimani akiendelea na matembezi yake ya ukaguzi wa mradi huo na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ. Mhe. Masoud Ali Mohamed, Waziri wa Maji na Nishati Mhe. Suleiman Masoud Makame na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliani na Uchukuzi Ndg. Amour Hamil Bakari.
MWANANCHI mkaazi wa Kikwajuni Ndg Adam Natepe akizungumzia kero ya Uwanja wa Mpira wa Mnazi Mmoja kujaa maji wakati wa mvua na kutoa mchango wake kuondoa kero hiyo, kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) wakati wa ziara yake kutembelea Mradi wa Huduma za Jamii Mjini (ZUSP) 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wananchi na Viongozi wa Serikali wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa Huduma za Jamii Mjini Zanzibar (ZUSP) katika maeneo ya mnazi mmoja wakati wa kumalizia matembezi ya ziara yake kukagua mradi huo, (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said
WANANCHI wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) wakati akizungumza na Viongozi na Wananchi juu ya ziara yake kutembelea na kujionea utekelezaji wa Mradi wa Huduma za Jamii Mijini Zanzibar (ZUSP) akimalizia matembezi ya ukaguzi wa mradi huo katika eneo la mnazi mmoja. Matembezi hayo yameazia barabara ya Kiembesamaki Uwanja wa Ndege ulikoazia mradi huo hadi mnazi mmoja.



 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.