RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa katika matembezi ya ziara yake
kutembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa Huduma za Jamii Mjini Zanzibar (ZUSP)
aliazia katika eneo la barabara ya
Kiembesamaki Uwanja wa Ndege kutembea na kujionea utekelezaji huo na kumalizia
matembezi hayo katika eneo la mnazi mmoja na kuzungumza na Uongozi unaosimamia Mradi huo, na (kulia kwa Rais)
Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud
Ali Mohamed na (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.
Idrisa Mustafa Kitwana, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi na Katibu wa
Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed Said
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo wakati akiwa katika
matembezi ya kukagua maendeleo ya Mradi wa Huduma za Jamii Mjini Zanzibar (ZUSP)
akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe.Idrisa Mustafa Kitwana,
wakiwa katika ziara hiyo kutembelea mradi huo wakipita katika eneo la Kilimani
na (kushoto) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akisisitiza jambo na kutowa maagizo wakati
wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa (ZUSP) akiwa katika eneo la kilimani
akiendelea na matembezi yake ya ukaguzi wa mradi huo na (kulia kwa Rais) Mkuu
wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana na (kushoto kwa
Rais) Waziri wa Nchi Tawala za Mikoa na Idara Maalum za SMZ. Mhe. Masoud Ali
Mohamed, Waziri wa Maji na Nishati Mhe. Suleiman Masoud Makame na Katibu Mkuu
Wizara ya Ujenzi Mawasiliani na Uchukuzi Ndg. Amour Hamil Bakari.
MWANANCHI mkaazi wa Kikwajuni Ndg Adam Natepe
akizungumzia kero ya Uwanja wa Mpira wa Mnazi Mmoja kujaa maji wakati wa mvua
na kutoa mchango wake kuondoa kero hiyo, kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi.(hayupo pichani) wakati wa ziara
yake kutembelea Mradi wa Huduma za Jamii Mjini (ZUSP)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Wananchi na Viongozi wa
Serikali wakati wa ziara yake ya kutembelea Mradi wa Huduma za Jamii Mjini
Zanzibar (ZUSP) katika maeneo ya mnazi mmoja wakati wa kumalizia matembezi ya
ziara yake kukagua mradi huo, (kulia kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi
Unguja.Mhe. Idrisa Mustafa Kitwana, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi
na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmed
Said
WANANCHI wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) wakati
akizungumza na Viongozi na Wananchi juu ya ziara yake kutembelea na kujionea
utekelezaji wa Mradi wa Huduma za Jamii Mijini Zanzibar (ZUSP) akimalizia
matembezi ya ukaguzi wa mradi huo katika eneo la mnazi mmoja. Matembezi hayo
yameazia barabara ya Kiembesamaki Uwanja wa Ndege ulikoazia mradi huo hadi
mnazi mmoja.
No comments:
Post a Comment