Habari za Punde

Ufunguzi wa Masjid Riyadhi Swaalihina Mgogono Wilaya ya Chakechake Pemba.

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, akifungua msikiti wa Masjid Riyadhi-Swaalihina Uliopo Mgogoni Wilaya ya Chake Chake, kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaji Dk.Hussein Ali Mwinyi.
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla (katikati), Mufti Mkuu wa Zanzibar Alhaj Shekh Saleh Omar Kabi, wakiwaongoza Viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wananchi wa Mgogoni katika sala ya Ijumaa, iliyosalishwa na Ustadhi Muhyiddin Makame Hamad, mara baada ya kuufungua masjid Riyadhu-Swaalihina Mgogoni
MWALIM Ali Juma Khamis akisoma risala ya wanakijiji cha Mgogoni Wilaya ya Chake Chake, kwa Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, baada ya kuufungua Rasmi Masjid Riyadhu-Swaalihina kwa niaba Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaji Dkt.Hussein Ali Mwinyi
MUFTI Mkuu wa Zanzibar Alhaj Shekh Saleh Omar Kabi, akitoa salamu zake kwa waumini wa dini ya Kiislamu kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, huko katika Masjid Riyadhu-Swaalihina Mgogoni Wilaya ya Chake Chake
MAKAMU wa Pili wa Rias wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, akitoa salamu za Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Alhaj Dkt.Hussein Ali Mwinyi, kwa wananchi wa Mgogoni, mara baada ya kuufungua Rasmi Masjid Riyadhu-Swaalihina Mgogoni Wawi Chake Chake Pemba.

VIONGOZI mbali mbali wa Serikali na wananchi wa kijiji cha Mgogoni Wilaya ya Chake Chake, wakifuatilia kwa makini ufunguzi wa Masjid Riyadhu-Swaalihina Mgogoni.

(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.