Habari za Punde

Kamati ya Bunge ya Miundombinu Yapata Semina Kuhusu Mawasiliano na Interneti

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile akitoa taarifa kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu huduma za mawasiliano na intaneti Bungeni, Dodoma. Aliyeketi wa pili kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula na wa kwanza kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Anne Kilango Malecela

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Seleman Kakoso akizungumza baada ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (aliyeketi mbele katikati) kuwasilisha taarifa kuhusu mawasiliano na intaneti kwa Kamati hiyo Bungeni, Dodoma. Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, akimsikiliza.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Anne Kilango Malecela akichangia mada baada ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa kwa Kamati hiyo kuhusu mawasiliano na intaneti Bungeni, Dodoma. 

Mbunge wa Ilala, Mussa Zungu akichangia hoja kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu baada ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa kuhusu mawasiliano na intaneti kwa Kamati hiyo Bungeni, Dodoma.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Dkt. Jabir Bakari akifafanua jambo kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu baada ya Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa kuhusu mawasiliano na intaneti kwa Kamati hiyo Bungeni, Dodoma.  Wa kwanza kulia ni Katibu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula na katikati ni Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.