USHAURI KWA UMMA
Katika
kuadhimisha Sikukuu ya Eid el Fitr, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais,
inachukua nafasi hii kutoa ushauri kwa wananchi juu ya kuchukua tahadhari
wakati wa mikusanyiko ili kuepuka maambukizo ya Virusi vya UKIMWI kwa kujiweka
mbali na mazingira yanayoweza kupelekea kufanya au kufanyiwa vitendo vya
udhalilishaji au kufanya ngono na mtu asiye stahiki.
Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais, inasisitiza kuchukua tahadhari kwa kufanya
yafuatayo:
1.
Epuka ngono, Usimuamini mtu.
Huenda akawa ameambukizwa VVU
2.
Epuka michanganyiko ya faragha
au sehemu zenye giza
3.
Jiepushe na unywaji wa pombe
na utumiaji wa dawa za kulevya unaweza kusababisha kuambukizwa VVU kwa kufanya
ngono zembe.
4.
Vaa kivazi cha stara kuepuka
kuvunjiwa heshima.
5.
Epuka matembezi wakati wa
usiku mkubwa
6.
Toa taarifa kwa vitendo
vyovyote vya udhalilishaji kwa mzazi na katika vyombo vya usalama
Tukiweza
kuyafanya haya, tutasheherekea sikukuu ya Eid el fitr kwa salama bila ya
maambukizo ya Virusi vya UKIMWI.
Kulu
A’amin wa Antum Bikhayr EID MUBARAK kwa
wananchi wote.
IMETOLEWA NA OFISI YA MAKAMU
WA KWANZA WA RAIS.
No comments:
Post a Comment