Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii Ruth Minja akieleza jinsi Tanzania inavyoendelea kudhibiti mfumuko wa bei ili kukuza uchumi na ustawi wa wananchi leo Julai 8, 2021 Jijini Dodoma wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuhusu mfumuko wa bei wa mwezi June, 2021.
Na Mwandishi wetu- Dodoma.
Tanzania imeendelea
kufanya vizuri katika kudhibiti mfumuko wa bei wa Taifa ikilinganishwa na nchi nyingine za Jumuiya ya Afrika Mashariki
kwa kipindi cha mwezi June , 2021.
Hayo yamesemwa na
Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii, Ruth Minja leo Julai 8, 2021 Jijini
Dodoma ambapo amesema mfumuko huo kwa
hapa nchini kwa mwezi Juni
umefikia asilimia 3.6 kutoka asilimia 3.3 mwezi Mei, Kenya 6.32 kutoka 5.87 ya
mwezi Mei, 2021 na Uganda 2.0 kutoka 1.9 mwezi Mei, 2021 .
“Ongezeko dogo la
Mfumuko wa Bei hapa nchini kwa mwaka unaoishia Mwezi Juni, 2021 unamaanisha
kuwa, kasi ya mabadiliko ya bei na huduma kwa mwaka unaoishia mwezi Juni, 2021
imeongezeka kidogo ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo mwaka ulioishia mwezi
Mei, 2021 na kwa nchi za Afrika
Mashariki Tanzania bado inafanya
vizuri”, alisisitiza Minja
Akifafanua amesema
kuwa Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuchukua hatua za kudhibi mfumuko wa
bei ili kuwawezesha wananchi kuendelea kuchangia
katika kukuza uchumi na shughuli
nyingine za maendeleo.
Baadhi ya bidhaa
zilizoongezeka bei kwa mwezi June ni; vitambaa vya nguo kwa asilimia 8.5, nguo
za wanawake kwa asilimia6.3, viatu vya wanawake kwa asilimia 6.3, viatu vya
wanaume kwa asilimia 6.2, kodi ya pango
asilimia 4.9, vyakula kwenye migahawa asilimia 5.6 na gharama za malazi kwenye
nyumba za kulala wageni kwa asilimia 5.7
Kwa upande wa bei za
vyakula na vinywaji Baridi kwa mwaka ulioishia mwezi June, 2021 umepungua hadi
asilimia 4.7 kutoka asilimia 4.9 kwa mwaka unaoishia mwezi Mei , 2021.
Ofisi ya Taifa ya
Takwimu (NBS) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa sheria ya Takwimu Sura
351 na yenye mamlaka ya kutoa, kusimamia na kuratibu upatikanaji na usambazaji
wa Takwimu rasmi.
No comments:
Post a Comment