Habari za Punde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Mhe Jamal Kassim Ali Amefanya Uteuzi wa Wajumbe wa Bodi ya ZSSF.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe.Jamal Kassim Ali, amewateua wajumbe  wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar  imesema, kwa mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 7(2), (c), (i), (ii), (iii) cha Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar Namba. 2 ya mwaka 2005, amewateua wafutao.

1. Bw.Arafat Ally Haji

2. Bw.Assaa Sharif  Khalid

3. Bw. Jaha Haji Khamis

4. Bi.Khadija Shamte Mzee

5. Bi. Sabra Omar Hussein

6. Bw.Said Abdalla  Basleym.

Uteuzi huo unaanza leo tarehe 20, July, 2021.

 

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.