Habari za Punde

Waziri wa Elimu Mhe Simai Mohammed Said Atembelea Skuli ya Ben Bella Kuangalia Maendeleo ya Ukarabati wa Majengo ya Skuli Hiyo.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe.Simai Mohammed Said akitowa maelekezo kwa Mjenzi wa ukarabati wa Skuli ya Sekondari ya Ben Bella wakati alipotembelea Skuli hiyo kujionea maendelea ya ujenzi huo.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe, Simai Mohammed Said amefanya ziara kuangalia maendeleo ya matengenezo ya Skuli ya Sekondari Benbella yaliyoanza mwezi wa Novemba mwaka jana chini ya kampuni ya ujenzi MODERN BUILDING CONTRACTORS,  ya hapa Zanzibar.

Mhe. Simai katika ziara hiyo amewataka wakandarasi wa ujenzi wa Skuli hiyo 
Kuhakikisha matengenezo hayo yanakuwa bora na  kumalizika kwa wakati.

Na Maulid Yussuf WEMA

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.