Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi
Jumuiya za Umoja wa Afrika ili kuendeleza utalii kwa lengo la kukuza uchumi wa
nchi wanachama.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maliasili na
Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) katika Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani 2021
yaliyofanyika Jijini Abidjan nchini Côte d' Ivoire leo.
“Lengo kuu la kushiriki katika Maadhimisho haya
ni kujifunza na kuangalia namna ya
kendeleza utalii wetu hasa katika kipindi hiki cha kukabiliana na janga Uviko
19 lililoikumba dunia”amesisitiza Mhe.
Masanja.
Aidha, Mhe. Mary Masanja ameongeza kuwa
ushiriki huo ni fursa ya kubadilishana uzoefu na pia kuvitangaza vivutio vya
Utalii vilivyoko nchini Tanzania ikiwa ni moja ya juhudi za kuunga mkono kazi
anayoifanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan
ya kutangaza utalii duniani.
Tanzania huadhimisha Siku ya Utalii Duniani
kila mwaka Septemba 27 na kauli mbiu ya Siku ya Utalii Duniani kwa mwaka huu ni
“Utalii
kwa Maendeleo Shirikishi/ Jumuishi”
No comments:
Post a Comment