Habari za Punde

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Mpango Atembelea Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere.

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor akitoa maelekezo kwa Waziri wa Nishati January Makamba wakati alipotembelea Jengo la Mitambo katika eneo la Ujenzi wa Mradi wa kufua umeme katika Bwawa la Julius Nyerere.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor akitoa maelekezo kwa Waziri wa Nishati January Makamba wakati alipotembelea Jengo la Mitambo katika eneo la Ujenzi wa Mradi wa kufua umeme katika Bwawa la Julius Nyerere.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akisikiliza maelezo kutoka kwa Waziri wa Nishati January Makamba juu ya maendeleo ya ujenzi wa kituo cha kupokea na kusafirisha  umeme kutoka katika mradi wa kufua umeme wa bwawa la Julius Nyerere. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akishuhudia maendeleo ya ujenzi wa njia kuu za maji ya kuendesha mitambo katika mradi wa kufua umeme wa Bwawa la Julius Nyerere.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Philip Isdor Mpango hii leo Oktoba 12,2021 ametembelea mradi  wa ujenzi wa Bwawa la Julius Nyerere katika mto Rufiji, mradi unaogharimu shilingi Trioni 6.58.

 

 

Akizungumza mara baada ya kutembelea mradi huo, Makamu wa Rais ameipongeza wizara ya Nishati, Wakandarasi pamoja na wafanyakazi wote wanaoshiriki katika ujenzi wa mradi huo. Amesema mradi huo ni mkombozi katika sekta ya nishati nchini hivyo amewataka viongozi na wote wanaohusika katika mradi huo kuwa wazalendo na kutanguliza maslahi ya taifa wakati wote.

 

Amesema dhamira ya serikali ni kuhakikisha mradi huo unakamilika kama ilivyopangwa na hivyo ameagiza wakandarasi kuwa makini na kutatuta hitilafu yeyote itakayojitokeza mapema ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza baadae katika mradi huo.

 

Katika hatua nyingine Makamu wa Rais ameagiza viongozi wa mikoa na wilaya zote inakopita mito inayotiririsha maji katika mto Rufiji kutunza mito hiyo na kutoa elimu kwa wananchi ili kulinda mazingira kwa manufaa ya mradi huo.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.