Habari za Punde

DC MOYO: Amepiga Marufuku Kuziba Vichochoro Manispa ya Iringa.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiona na baadhi ya wananchi wa manispaa ya Iringa wakati wa ziara ya kusikiliza kero za wananchi wa wilaya hiyo
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto
Baadhi ya vichochoro ambavyo vimezibwa kwa kuta na mageti na kuhatari maisha ya wananchi wengine endapo itatokea majanga yoyte yale hasa moto


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ametoa amri ya kuvunjwa kwa kuta zote zilizojengwa kuziba vichochoro katika maeneo ya makazi ya watu Manispaa ya Iringa wavunje mara moja kabla sheria haijachukua mkondo wake kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria za nchi.

Moyo alitoa amri hiyo baada ya kufanya ziara katika baadhi ya mitaa ya kati kati ya mji wa Iringa na kubaini kuzibwa kwa vichochoro jambo ambalo amelitaja kuwa ni kinyume na sheria za mipango miji.

Wakati wa ziara hiyo iliyofuatiwa na mkutano wa hadhara katika kata ya Mivinjeni Moyo amesema kuzibwa kwa vichochoro kunakwamisha jitihada za uokoaji nyakati yanapotokea majanga ya moto hali inayohatarisha usalama.

Alisema kuwa kumeibuka tatizo la wananchi kuziba vichochoro vilivyopo mtaani bila kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika.

Moyo alisema kuwa wananchi wote walioziba vichochoro watachukuliwa hatua kali za kisheria kwa kuwa wanafanya makosa hayo makusudi hivyo wanapaswa kuvunja mara moja ili kuweka mitaa yote katika hali ya usalama.

Alisema wananchi wote wanaofanya shughuli za ujenzi  wanatakiwa kuwa na kibali kutoka katika mamlaka husika la sivyo watakukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa wanakuwa wamevunja sheria kwa makusudi.

Moyo alisema kuwa vichochoro vyote vilivyopo manispaa ya Iringa vinatakuwa kuwa wazi na marufuku wa idara ya mipango miji kutoa kibali cha kuziba vichochoro kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi wa manispaa ya Iringa na nje ya Iringa.

Alisema kuwa ukitokea moto inakuwa vigumu kuuzima kutokana na kuziba kwa vichochoro na kuleta madhara kwa wananchi ambao wanakuwa wamepata majanga hayo kwa kujitakia.

Moyo aliwataka wafanyakazi wote wa manispaa ya Iringa kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwa kuwa serikali haijawahi kwenda likizo hivyo wafanyakazi wanatakiwa kuwa kazini muda wote.

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo anatoa agizo hilo ikiwa ni siku ya pili mara baada ya kuanza ziara katika manispaa ya Iringa na kubaini kuwepo kwa changamoto ya kuzibwa kwa vichochoro vinavyopaswa kuwapo kati ya jengo moja na jingnine

Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya Makusudi ya amri hii aliyoitoa ni kuyafanya makazi ya watu katika manispaa ya Iringa kuwa maeneo salama na hasa akieleza kuachwa wazi kwa maeneo hayo kutarahisisha shughuli za uokoaji pindi majanga ya moto yanapotokea

Hata hivyo anawageukia maafisa wa Idara ya Mipango miji Manispaa ya Iringa akiwaonya kuwa endapo wamehusika kuruhusu kuzibwa kwa vichochcoro hiyo hatua kali zitachukuliwa huku akiwahusisha na Rushwa

Mkuu huyo wa Wilaya anasema ni jambo la kushangangaza kuona wataalam wa Idara ya Mipango miji pamoja na viongozi wa Serikali za mitaa na kata kwa kushindwa kuchukua hatua licha ya kushughudia kila kukicha vichochcoro vikiendelea kuzibwa huku akiwataka kuasha kufanya kazi kwa mazo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.