WAZIRI wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita ameuagiza uongozi wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi pale linapotokea tatizo au hitilafu yeyote ya kiufundi.
Kauli hiyo ameitoa baada ya kufanya ziara ya kuangalia hali halisi iliyojitokeza baada ya kuathirika kwa baadhi ya maeneo kufuatia radi na mvua kubwa iliyonyesha mwezi uliopita.
Alisema Serikali na Wizara inatambua changamoto zinazowakabili Shirika hilo katika uendeshaji baada ya kuharibika baadhi ya vifaa ,hivyo amewataka wafanyakazi kuwa watulivu huku jitihada kubwa zinachukuliwa katika kuhakikisha matangazo yaliyojitokeza yanatatuliwa.
Waziri Tabia alisema kuna changamoto ambazo zimetokea za kitaalamu ambazo hazihitaji wataalamu wa ndani bali ata wa nje ya Zanzibar ambapo mda wowote ndani ya wiki hii watawasili ili kusaidia tatizo hilo.
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika hilo Salum Ramadhan amewataka wananchi kuwa na subra kwani jitihada zinachukuliwa ili ZBC kurejesha matangazo yake yatakayo kuwa na ubora zaidi.
Kwa upande wake fundi wa ZBC ambaye pia Mkuu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Tehama Iddi Mohamed alisema wanatarajia kupokea wataalamu hivi karibuni kwa ajili ya kufanya matengenezo ya baadhi ya vifaa vilivyoharibika.
No comments:
Post a Comment