Waziri wa Nchi Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Harusi Said Suleiman amesema kuwa mashirikiano
ya pamoja yanaleta maelewano katika sehemu ya kazi na kukuza uhusiano mwema
unaojenga imani na mapenzi baina yao
Mhe Harusi ameyasema hayo wakati alipofanya
mazungumzo na wafanyakazi wa ofisi hio kwenye ukumbi wa mkutano uliopo
Migombani na kuwasisitiza kuwa suala la nidhamu na heshima katika kazi ni jambo
la msingi huku wakijua kuwa taifa linawategemea
Bi Harusi amesisitiza
kuwa mashirikiano ya wenyewe kwa wenyewe yanawaleta karibu wafanyakazi na
watendaji jambo ambalo linaleta ufanisi katika sehemu za kazi ndipo mipango ya
utekelezaji na ujenzi wa taifa inapoendana na kasi ya utendaji
“hakikisheni mnajikita
katika majukumu ya kazi na mmoja wenu anapoondoka majukumu hayalali bali kazi
iendelee ndio maana nawasisitiza kupendana pia msifanye kazi kwa mazowea badala
yake jitahidini kuleta ufanisi ili maendeleo yaweze kupatikana” alisisitiza Mhe
Harusi
Aidha Bi Harusi
amewakumbusha wafanyakazi kuzingatia muda wa kuingia na kutoka kazini na
inapotokea hali ya dharura kutoa taarifa kwani si vyema kunyamza unaweza
kupoteza haki zako za msingi mambo ambayo hayana tija kiutendaji
Kuhusu suala la
uwajibikaji amewataka wafanyakazi kuhakikisha wanatoa huduma stahiki kwa jamii
hivyo kila mfanyakazi afahamu majukumu yake pamoja na kuzingatia suala la
utowaji wa huduma kwa walioko nje ya ofisi kuhakikisha wanafikiwa
Nae Katibu Mkuu Ofisi
ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar D. Shajak amemuhakikishia Mhe Waziri kuwa
nidhamu na mashirikiano ndio yenye kuleta uhai wa taasisi jambo viongozi wa
Ofisi hio wanalisisitiza kwa watendaji na wafanyakazi wote
No comments:
Post a Comment