RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Taifa kuhusu “Generation Equality Forum” Mhe. Angela Kariuki, akitowa maelezo ya Kazi ya Kamati hiyo wakati wa mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar,akiwa na Ujumbe wake walipofika kujitambulisha leo 15-6-2022, (kulia kwake) Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mgeni Hassan Juma.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Kamati ya Ushauri ya Taifa kuhusu”Generation Equality Forum, ukiongiozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe Angela Kariuki (kulia kwa Rais) mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 15-6-2022, walipofika Ikulu kwa mazungumzo na kujitambulisha.
RAIS
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi
akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Kamati ya Ushauri ya Taifa kuhusu
“Generation Equality Forum” baada ya kumaliza mazungumzo yao walipofika Ikulu
Zanzibar leo. Angela Kariuki15-6-2022.(Picha na Ikulu)
Alieleza
kufurahishwa na utaratibu wa kupata matokeo yanayotarajiwa kwani ni njia nzuri
ya kupata matokeo yanayotarajiwa na pia, ni njia nzuri za kufanya tathmini.
Aliupongeza
Mpango wa Kamati hiyo kwa kujikita na mambo muhimu na kueleza kwamba juhudi za
makusudi zitafanyika katika kuhakikisha bajeti maalum inawekwa kwa Wizara
husika ili kufanikisha Mpango huo.
Mapema,
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Angellah Kairuki alitumia fursa hiyo kuitambulisha
Kamati pamoja na kumjuulisha Rais jitihada zilizofanyika tangu kuzinduliwa
rasmi kwa Kamati hiyo na Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania mnamo Disemba 16, 2021 huko Jijini Dodoma.
Alisema kuwa
katika kuhakikisha utekelezaji wa ahadi za nchi, Kamati hiyo ya Ushauri ya
Kitaifa yenye wajumbe 25 kutoka Serikalini na Asasi za Kiraia, Taasisi za Elimu
ya Juu, Taasisi za Utafiti na Sekta binafsi ambapo wajumbe 19 kutoka Tanzania
Bara na 6 kutoka Zanzibar imeundwa ili kushauri jinsi ya kuhakikisha ahadi za
nchi zinafikiwa.
Mwenyekiti huyo
alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kuunda Wizara inayojitegemea
inayoshughulikia masuala ya Jinsia, Wazee na Watoto kwani ni chombo muhimu sana
katika haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake.
Aidha,
alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kuendelea kuwa kinara na mhamasishaji wa
kampeni ya ‘He for She’ ambayo ni mkakati muhimu sana katika usawa wa
jinsia na uwezeshaji wanawake.
Sambamba na
hayo, Mwenyekiti Kairuki alimuhakikishia Rais Dk. Mwinyi kwamba Kamati hiyo iko
tayari kufanya kazi na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kuhakikisha
inapata matokeo tarajiwa.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano,
Ikulu Zanzibar. OF
RESPONSIBILITY
No comments:
Post a Comment