STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 30, Agost, 2022
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi amesema ushiriki wa Taasisi zisizo za kiserikali katika uimarishaji
wa huduma za Kijamii ni muhimu, kwa kuzingatia kuwa Serikali haina uwezo wa
kuwafikia wananchi wote.
Dk. Mwinyi amesema hayo Ikulu
Zanzibar, alipozungumza na Viongozi wa Taasisi za Milele Zanzibar Foundation na
IFRAJ waliofika kumsalimia pamoja na kuelezea kwa kkna shughuli mbali mbali
zinazofanywa na Taasisi hizo.
Amesema kwa kipindi kirefu sasa
taasisi hizo zimekuwa zikifanya kazi kubwa ya kuisaidia Serikali, hususan
katika uimarishaji wa sekta za huduma ya jamii.
Alizipongeza Taasisi hizo kwa kufanya
kazi kubwa na kuwa taasisi zinazofanya
vyema zaidi hapa nchini katika kuisaidia Serikali katika uimarishaji wa sekta
za huduma za jamii, ikiwemo Afya, elimu, maji na Uwezeshaji wajasiriamali.
.
“Ninaridhika na kazi kubwa mnayofanya
kwa kuwa inagusa vipaumbele vya Serikali katika kuimarisha huduma za jamii”,
alisema.
Alieleza kufurahishwa kwake na kazi
kubwa inayofanywa na taasisi hizo katika kujenga mifumo pamoja na kuzingatia
umuhimu wa ujenzi wa miundombinu, uwepo wa rasilimali watu na mahitaji ya vifaa
katika sekta hizo.
Dk. Mwinyi alieleza kuwa Zanzibar
inakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa maji safi na salama, hivyo hatua
inayochukuliwa na taasisi hizo ya kusaidia upatikanaji wa Pampu pamoja na
uchimbaji wa visima ni ya kupongezwa.
Alipongeza taasisi ya IFRAJ kwa
ujenzi wa nyumba 500 za makaazi ya
binadaamu na kusema hatua hiyo ni muhimu katika kuisaidia jamii.
Aidha, alitoa shukrani kwa ujenzi wa Misikiti na
Madrasa katika maeneo mbali mbali hapa nchini, na kusema hatua inasaidia uendelezaji wa Dini ya
Kiislamu.
Rais Dk. Mwinyi alisema Serikali
itatoa msukumo ili kufanikisha ujenzi wa Barabara ya Birikau Kisiwani Pemba
pamoja na kuuagiza Uongozi Kikosi cha
Kuzuia Magendo KMKM kutoa elimu kwa wamiliki wa Boti za kusafirishia wananchi
katika maeneo ya Visiwa Kisiwani Pemba, ili kuwahakikishia usalama katika
safari za baharini.
Mapema, Mkuu wa Miradi wa Taasisi ya Milele
Zanzibar Foundation Khadija Ahmeid Sharrif alisema taasisi hiyo imekuwa mstari
wa mbele katika kuisaidia jamii kupitia sekta mbali mbali, ikiwemo ya
uimarishaji wa Afya, elimu, maji pamoja na uwezeshaji Ujasiriamali.
Alisema taasisi hiyo imekuwa
ikisaidia uimarishaji wa Afya ya mama na mtoto kwa kuendeleza ujenzi wa Vituo
vya Afya katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba, kusaidia vifaa vya tiba
pamoja na kuwajengea uwezo wafanyakazi wa sekta hiyo.
Aidha, alisema Taasisi hiyo inatoa msukumo
mkubwa katika maendeleo ya sekta ya
elimu nchini kwa kufanikisha ujenzi wa majengo ya skuli pamoja na kutoa kusaidia
upatikanaji wa mbinu sahihi za kufundishia ,pamoja na kufanya tafiiti.
Vile vile alisema taasisi imekuwa
mstari wa mbele katika kuwawezesha wajasiriamali, wakiwemo akinamama na vijana
katika kustawisha kilimo cha zao Mwani pamoja na kulifanyia usarifu wa zao hilo
ili kuwaongezea kipato.
Nae, Meneja wa taasisi ya IFRAJ
Abdalla Said Abdalla alisema taasisi hiyo imekuwa ikijishughulisha na ujenzi wa
nyumba za makaazi kwa wananachi wenye kipato cha chini, ambapo hvii sasa
wanakamilisha ujenzi wa nyumba 500 zinazogharimu zaidi ya shilingi Bilioni 7.5.
Aidha, alisema taasisi hiyo pia
imekuwa ikijishughulisha na ujenzi wa nyumba za Ibada ikiwemo Misikiti na
Madrasa katika maeneo mbali mbali nchini, kusaidia wajene na mayatima pamoja na
kutoa chakula kwa wanafunzi wa tutu.
Vile vile imekuwa ikisadia ujenzi wa Kliniki, ujenzi wa
majengo ya skuli, kuimarisha upatikanaji wa huduma za maji safi na salama kwa
kuchimba visima na kusaidia upatikanaji wa Pampu pamoja na kusaidia huduma
muhimu wakati wa majanga, ikiwemo matukio ya moto.
Katika hatua nyengine, Ahmeid aliomba
Serikali kusaidia Wataalamu watakaoweza kutoa elimu kwa wamiliki wa Boti za
kusafirishia wananchi kwenye Visiwa ili kuepusha ajali, huku akibainisha azma
ya taasisi hiyo kusaidia upatikanaji wa Vazi la Uokozi (life Jacket).
Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment