Idara ya Menenjimenti ya Maafa imefanya semina ya kuwajengea uwezo wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Muswada wa Sheria ya Usimaizi wa Maafa ili kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu sheria na namna zinavyofanya kazi pindi maafa yanapojitokeza.
Semina hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Bunge Jijini Dodoma ikihusisha wajumbe wote wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria iliyoandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu.
Idara ya Menejimenti ya Maafa kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imepewa jukumu la kuratibu na kushughulikia maafa na dharura zote ikijumuisha shughuli za Kuzuia, Kujiandaa, Kukabili na Kurejesha hali.
Viilevile Shughuli za kila siku za Idara zinaongozwa na Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya mwaka 2004 na sheria ya Menejimenti ya Maafa Na.7 ya mwaka 2015.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Joseph Mhagama akifafanua jambo wakati semina hiyo.
Sehemu ya Wakuu wa Idara kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia semina hiyo katika Ukumbi wa Bunge Agosti 31, 2022 Jijini Dodoma.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
No comments:
Post a Comment