Habari za Punde

WADAU WAKUTANA KUJADILI AFUA YA AFYA MOJA.

 

Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Luteni Kanali Selestine Masalamadu akifungua warsha ya Uchambuzi wa Gharama na Manufaa ya Utekelezaji wa Dhana ya Afya Moja nchini iliyofanyika  Jijini Dodoma.

Na Mwandishi wetu-Dodoma

Kikao cha Uchambuzi wa Gharama na Manufaa ya Utekelezaji wa Dhana ya Afya Moja nchini ambayo lengo lake ni kukabiliana na magonjwa yanayowakumba bindamu, wanyama na mimea.

Kikao hicho kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia Septemba 8 hadi 9 mwaka huu  kilifunguliwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Luteni Kanali Selestine Masalamadu na kuhudhuriwa na  wadau mbalimbali wa maendeleo.

 Aidha  kinalenga kufanya uchambuzi huo ili kuonesha thamani yake na kuvutia uwekezaji wa rasilimali kutoka kwa serikali na wadau mbalimbali wa afya moja.

Mshauri kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) Dkt. Janeth George  (aliyesimama) akiwasilisha taarifa ya Uchambuzi wa Gharama na Manufaa ya Utekelezaji wa Afya Moja nchini.

Baadhi ya washiriki wa wakifuatilia kikao hicho kilichofanyika Jijini Dodoma.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.