Habari za Punde

Waziri Mkuu atoa mkono wa pole kwa familia ya Rais Dk Hussein Mwniyi

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Kassim Majaliwa akisalimiana na kutowa mkono wa pole kwa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi kwa kufiwa na Mtoto wake Hassan Ali Hassan Mwinyi, alipofika nyumbani kwa marehemu Chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 2-9-2022. na (kulia kwa Mzee Mwinyi) Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi.(Picha na Ikulu)
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Kassim Majaliwa akitowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi Mtoto wa Rais Mstaafu wa Tanzania Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, alipofika nyumbani kwa marehemu Chukwani Wilaya ya Magharibi "B"Unguja leo 2-9-2022, kwa ajili ya kutowa mkono wa pole..(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi na Rais Mstaafu wa Tanzania Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi, wakipokea mkono wa pole kutoka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Kassim Majaliwa, alipofika nyumbani kwa Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi Chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja kutowa mkono wa pole kwa Familia ya marehemu leo 2-9-2022.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj.Dk.Hussein Ali Mwinyi na (kushoto kwa Rais)  Rais Mstaafu wa Tanzania Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Kassim Majaliwa wakiitikia dua ya kumuombea Marehemu Hassan Ali Hassan Mwinyi ,ikisowa na Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume, baada kutowa mkono wa Pole kwa Familia ya marehemu nyumbani kwake chukwani Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 2-9-2022.(Picha na Ikulu)

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

 

Zanzibar                                                                           02 Septemb

 

WAZIRI Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Majaliwa Kassim Majaliwa leo  ameifariji Familia ya Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Ali Hassan Mwinyi kutokana na kifo cha mtoto wake Hassan Ali Hassan  kilichotokea Jumatano wiki hii katika Hospitali Kuu ya Mnazi mmoja, Mkoa wa Mjini Magharibi.

 

Hafla  hiyo ilioambatana na Dua ilifanyika nyumbani kwa Marehemu Chukwani Mkoa Mjini Magharibi ambapo Waziri Mkuu pia alipata fursa ya kutoa mkono wa pole kwa  Rais mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, Mama Siti Mwinyi, Mke wa marehemu Fauzia Salim Hilali pamoja na wanafamilia.

 

Waziri Mkuu Majaliwa alimuomba Mwenyezi Mungu amsamehe madhambi yake marehemu, huku akiwataka wafiwa kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wao.

 

 

Imetayarishwa na Idaya 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.