Habari za Punde

Uzinduzi wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi


 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi Tanzania ni muhimu kwani utawezesha Serikali na Wadau tofauti kupata hali halisi ya mwenendo wa maradhi hayo na kusaidia kuweka mikakati ya kwenda sambamba na uhalisia katika kupambana na tatizo hilo.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko hotel ya Verde Mtoni wilaya ya Magharibi ‘A’ Mkoa wa Mjini Maghari alipozungumza katika uzinduzi wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya Ukimwi nchi utakaofanyika Tanzania Bara na Zanzibar.

Amefahamisha kwamba kupatikana kwa takwimu sahihi ni silaha muhimu katika kupanga na kuaandaa mikakati  ya kupambana na maradhi hayo kwa kuwa itasaidia kufahamika mwendendo wa tatizo hilo kwa ukamilifu kote nchini.

Hata hivyo, Mhe. Othman amesema kwamba kwa upande wa Zanzibar ni vyema utafiti huo kwenda sambamba na utafiti wa viashiria vya  Maambukizo ya Virusi vya Ukimwi kwa kuhusisha makundi maalum ambayo yanaaminiwa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya maradhi hayo ikilinganishwa na jamii ya kwaida.

Amefahamisha kwamba utafiti huo utahusisha Kaya zipatazo 20 alfu  kwa Tanzania Bara na Zanzibart  na kuwataka wananchi kuondoa hofu juya suala hilo na kuwataka kuona kwamba kaya zote zina fursa  sawa ya kushiriki kwenye utafiti huo.

Mhe. Makamu amesema kwamba kwa ujumla inatarajiwa kwamba utafiti huo utahusisha watu wapato 40 alfu  kushiriki kwa utafiti wa mwaka 2022/2023 na kwamba ni matumaini ya serikali kwamba kaya zilizochaguliwa  na watu watakaohusika watatoa ushirikiano wa kutosha katika kufanikisha suala hilo muhimu na kwamba taarifa zitakazopatikana zitaendelea kuwa siri na zitatumika kitakwimu pekee.

Amesema kwamba Tanzanzia inayo mikakati kadhaa ya kupambamba na tatizo hilo kwa kuwa ni muhimu pia katika kusaidia nchi kupiga hatua kiuchumi kuwa kuwepo jitihada na mikakati imara ili wananchi waepukane na maradhi ikiwemo janga la Ukimwi.

Mhe. Othman amezishukuru serikali ya Marekani kupitia kituo chake cha Kudhibiti na kuzuia Magonjwa  kwa kuendelea kuisaidia nchi Kitaalamu na Kifedha  kuweza kufanya utafiti huo muhimu katika kupambana na maradhi ya Ukimwi. 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar Dk. Ahmed Khatib, amesema kwamba Zanzibar kumekuwa na mkikakati mbali mbali mbali ambayo imesaidia sana katika kupambana na kudhibiti janga hiloi tokea ilipobainika mgonjwa wa kwanza mwaka 1986 hapa Zanzibar.

Naye Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndugu Salim Kassim Ali, asmesema kwamba utafiti huo utawahusisha watu kuanzia umari wa miaka 15 na kuendelea  na kwamba takwimu zitakazopatikana zitasaidia sana katika kubuni sera mpya na kupanga mikakati zaidi ya kupambana na janga hilo.

Utafiti huo unasimamiwa kwa pamoja kati ya Tume ya Ukimwi Zanzibar na Tanzania Bara, Ofisi za Mtakwimu Mkuu wa Zanzibar na Tanzania Bara pamoja na mashirika mbali mbali ya kimataifa ikiwemo Marekani, Who  na mengineyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.