Habari za Punde

Ufunguzi wa mkutano wa Kimataifa kuhusu kubadilishana taarifa na uzoefu kwa uhalifu unaochupa mipaka

 

NA OMAR HASSAN – ZANZIBAR                                                 22/11/2022

Kamishna wa Intelijensia ya Jinai, Charles Mkumbo amefungua mkutano wa Kimataifa kuhusu kubadilishana taarifa na uzoefu kwa uhalifu unaochupa mipaka huko Michamvi Mkoa wa Kusini Unguja Visiwani  Zanzibar .

Amesema Mkutano huo ni fursa muhimu kwa nchi washiriki kubadilishana uzoefu katika kuzuwia na kukabiliana na changamoto za kiusalama hasa kwa uhalifu unaovuka mipaka.

Mkutano huo wa siku tatu umezishirikisha nchi ya Gabon, Congo DRC, Malawi, Niger, Uganda na wenyeji Tanzania na kufadhiliwa na Umoja wa Nchi za Ulaya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.