Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) akizungumza na Madaktari wa Kichina waliofika Ikulu Jijini Zanzibar kujitambulisha leo, wakifuatana na Balozi Mdogo wa China anayefanyia kazi Zanzibar Mhe.Zhang Zhisheng (wa pili kulia)
RAIS wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa timu
ya madaktari bingwa kutoka China ni faraja na fursa adhimu ya kuimarisha sekta
ya Afya Zanzibar.
Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu, Zanzibar alipozungumza
na timu ya madaktari hao walioongozwa na Balozi Mdogo wa China anayepo
Zanzibar, Zhang Zhisheng chini ya kiongozi wa madaktari hao Dk. Zhao walipofika
kujitambulisha.
Alisema ushirikiano uliopo baina ya China na Zanzibar ni
wa kihistoria na wa muda mrefu, na aliishukuru Serikali ya China kwa kuendelea
kuiungamkono Zanzibar hususan kwenye sekta ya afya, kwa msaada wa vifaa vya
kisasa na teknolojia mpya ya kufanya operesheni bila upasuaji pamoja na huduma
nyingine za uchunguzi na kitabibu.
Rais, Dk. Mwinyi aliwapongeza madaktari hao kwa kazi
nzuri wanayoifanya Zanzibar ya kuwahudumia wananchi kwa kuwatibu kwa kutumia
utaalamu wa kisasa. Alisema Madaktari hao mbali ya kutoa mbinu za kibingwa pia
wanasaidia maeneo mbalimbali ya afya ikiwemo kutoa vifaa vya kisasa kwenye
hospitali hizo, utaalamu kwa madaktari wazawa na kuweka miundombinu sawa ya
hospitali.
Dk. Mwinyi aliiomba serikali ya China kuisaidia Zanzibar
madaktari bingwa kwani serikali imejiimarisha zaidi kwenye sekta ya Afya kwa
kuongeza hospitali za wilaya Unguja na Pemba hivyo, aliwaomba madaktari
hao kuongeza nguvu na utaamu kwenye
hospitali hizo.
Akizungumza
kwenye hafla hiyo, Balozi mdogo wa China, Zhang Zhisheng alimpongeza Rais Dk.
Mwinyi kwa kuiongoza Zanzibar kuwaletea maendeleo wananchi wake na kueleza
wanashuhudia mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar.
Naye
Waziri wa Afya, Nassor Ahmed Mazrui, aliishukuru timu ya madaktari hao kwa
kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na kukubali kujitoa kuongeza nguvu
kuimarisha sekta ya afya nchini.
Naye,
Mkurugenzi wa tiba Wizara ya Afya Dk. Msafiri Marijani alieleza madaktari hao
ni wataalamu wa masuala ya ENT, operesheni kwa kinamama bila kupasua, macho,
meno, uzazi na magojwa megine ya kinamama, wataalamu wa mionzi pamoja na wa
uchunguzi wa magonjwa ya kansa pamoja na wakalimali ambao watakuwepo Zanzibar
kwa mwaka mmoja wakishirikiana nao kwenye hopaitali za Mnazi Mmoja na Abdalla
Mzee, Pemba pamoja na kuongeza nguvu na utaalamu kwa hospitali za Kivunge na
Chakechake Pemba.
Dk.
Marijani alieleza mafanikio makubwa yamepatikana kutokana na ujio wa madaktari
wao mbali na matibabu kwa wananchi lakini kuanzishwa kitengo cha madaktari
bingwa watakaofanya oparesheni bila ya kumpasua mgonjwa katika hospitali za
Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee.
Alisema
kwa mara ya kwanza Mnazimmoja wametumia upasuaji bila kupasua ambao ulifanikiwa
kwa kiasi kikubwa. Sambamba na kusifu vifaa vipya vya kitaalaamu kutoka kwa
timu hiyo aliyoieleza kwamba imeongeza uweledi na ufanisi wa hali ya juu.
Akizungumza
kwenye hafla hiyo, kiongozi wa timu ya madaktari hao, Dk. Zhao waliishukuru
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na uongozi wa Wizara ya Afya kwa ushirikiano
waliowaonesha tokea wamefika Zanzibar mwenzi Septemba mwaka jana pamoja na
kusifia ukarimu wa watu wa Zanzibar waliobahatika kukutaana nakueleza hakika ni
watu wakarimu na wenye kuenzi utamaduni, umoja na upendo kwa wageni.
Dk.
Zhao ambae pia ni mtaalamu wa upasuaji wa magonjwa yote, alieleza kipindi
kifupi walichofika Zanzibar kwa ushirikiano wa madaktari wenyeji wa Mnazi Mmoja
na Abdalla Mzee wamefanikiwa kutibu wagonjwa wengi wa maradhi mbalimbali na
kufanikiwa kutibu kesi nyingi zilizokua zikiwasumbua wananchi wa Zanzibar
waliofika vituo humo kwaajili ya matibabu.
Alieleza
anatumai uwepo wao utapunguza kesi nyingi ninazowasumbua wananchi na kuwataka
kuitumia fursa ya uwepo kwa kufika kwa
wingi kwenye hospitali za umma ili wapate matibabu na ushauri wa kitaalam
Timu ya madaktari bingwa 32 kati yao 12 watashirikiana na
madaktari wazawa kwenye Hospitali kuu ya Mnazi Mmoja na madaktari tisa
watakwenda kuongeza nguvu kwenye hospitali ya Abdalla Mzee, Pemba kwa kufanya
kazi begakwa bega baina yao.
IDARA YA MAWASILINO, IKULU ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment