Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhajj Othman Masoud Amejumika na Wananchi na Viongozi Katika Iftari Iliyoandaliwa na Ofisi yake

 

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Alhaj Othman Masoud Othman, akizungumza wakati wa hafla ya Iftari iliyoandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kwa Viongozi wa Serikali, Dini,  Vyama vya Siasa na Watu Mashuhuri mbali mbali, iliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Alhaj Othman Masoud Othman, akisalimiana na kuagana na Kiongozi wa ACT-Wazalando Mhe Juma Duni baada ya kumalizika kwa hafla ya iftar aliyoandalia na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais   katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil, Wilaya ya Mjini Unguja.

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman  amesema kwamba ni vyema kwa Viongozi wenye dhamana na dhima mbali mbali nchini kuyachukuwa kivitendo mafunzo ya imani na nidhamu yanayopatikana ndani ya Mwezi mtukufu ili kuifanya Zanzibar kuepukana na masuala mbali mbali yanayoirejesha nyuma  kwa kuamini kwamba Mwenyezi Mungu yupo wakati wote.

Mhe. Othman ameyasama hayo huko katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdul -Wakili Kikwajuni Mjini Zanzibar alipowasalimia viongozi na wananchi mbali mbali mara baada ya kukamilika futari ya pamoja iliyoandaliwa na ofisi yake na kujumuisha wananchi mashuhuri wakiwemo mawaziri na viongozi mbali mbali.

Mhe. Makamu amesema kwamba mikusanyiko ya kibaada ikiwemo futari ya pamoja  wanayokaa wananchi na waumini mbali mbali inasaidia sana kuvunja na koondosha mambo  yanayotenganisha wananchi na kuongeza ihsani miongoni mwao  ikiwa ndiko kuuthamini msingi wa kuwa pamoja na kupata fadhala nyingi kutoka kwa mola muumba.

.Mhe Makamu amesema kwamba mikusanyiko ya namna  hiyo ni muhimu na inatoa fadhila nyingi za mwezi mtukufu wa ramadhani na  kuweza kutumia fursa ya mwezi mtukufu wa ramadhani kwa mja kuomba msamaha kwa  aliyokosea na kuwa na uhakika wa msahaha ikiwemo kupata fadhila na darja kubwa ukiwemo usiku mtukufu wenye kheir nyingi zaidi wa laylatul-kadri.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba ni wajibu wa waumini kumshukuru Mola muumba na kuwakumbusha wananchi  na waumini wa Kiislamu kwamba, mbali ya fadhila  za ramadhani zilizowekwa na Mola muumba, lakini pia mwezi huo ni chuo muhimu cha elemu ya kujenga nidhamu ya yakini kwa mwenyezimungu muumba.

Amesema kwamba suala la kujengeka nidhamu miongoni mwa waumini na wananchi  linasaidia sana taifa kupiga hatua na kupata maendeleo  na kamwe hakuna mwananchi ama kiongozi anayeweza kufanikiwa kwa lolote bila kufuata nidhamu  na kwamba mwezi mtukufu wa ramadhani unatoa funzo kubwakwa  jambo hilo sambamba na yakini ya kumcha mungu na kutegemea malipo yake.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba kufunga mwezi wa mtukufu wa ramadhani kwa waumini ni kutekeleza kwa  vitendo elimu ya nidhamu  katika kiwango cha juu cha mafunzo yatokanayo na ramadhani na kwamba waumini kuacha vyakula vya halali kwa kumuogopa  mola wao na kutarajia fadhila za mwezi mtukufu wa ramadhani ni jambo kubwa ambalo waumini wanapaswa kuliendeleza hata baada ya mfungo wa ramadhani.

Mhe. Othman amesema kwamba ni vyema kwa waisalamu wote kuiendeleza nidhamu inayopatikana katika mwezi mzima wa ramadhani ili wananchi na waislamu kwa jumla waoneshe kuhitimu kwao mafunzo yaliyopatikana mwezi wa ramadhani na elimu hiyo  iweze kuwa na manufaa zaidi duniani na kesho akhera.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mjini Mgharib Mhe. Idrisa Kitwana Mustafa akitoa salamu za mkoa baada ya futari hiyo,  ameitaka jamii kukemea maovu yaliyomo ndani ya maeneo yao   hasa sauala ya kuwepo madanguro  na upigaji wa muziki bila kufuata taratibu jambo ambalo ndio chachu ya maovu mengi kutokea na linaleta kero kubwa kwa wananchi na waumini  na wananchi mbali mbali..

Mhe. Kitwana amesema kwamba mwezi huu wa ramadhani ni mwezi wa kuchuma kheir na kujifunza zaidi kusoma ili itoe nguvu ya kuweza kuyaona mabaya zaidi na kuweza kujipendekeza kwa Mwenyezi Mungu Muumba kupata fadhila njema.

Amewataka wananchi kushikamana na kupendana kwa wema na kukumbushana katika mema na kuachana na mabaya na kuwaomba wananchi wote wa kukema vitendo vya ushoga ambavyo  vimekuwa vikishamiri kutokana na kuhamasishwa sehemu nyingi duniani .

Amewataka  wananchi wa Zanzibar kupambana kwa kukema suala la vitendo vya namna hiyo  unaotangazwa na baadhi ya mataifa duniani na kutaka wananchi wote walaani na kwamba viongozi kwenye mitaa wasiruhusu  kuwepo madanguro na upigaji wa madisko bila kufuata taratibu na maelekezo  ya serikali.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kutopitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 01.04.2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.