Habari za Punde

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Ndg.Abdulraham Kinana Amekutana na Kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara Ndg. Abdulrahman O. Kinana ameongoza Ujumbe wa CCM kwenye mazungumzo na Mhe. Vo Van Thuong, Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Jijini Ha Noi, Viet Nam.

Katika mazungumzo hayo, Ndg. Kinana aliwasilisha ujumbe maalum kutoka kwa Mhe Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, wa kuhimiza ushirikiano wa kiuchumi baina ya nchi  hizo mbili ili kuwanufaisha wananchi wa Tanzania na Vietnam.



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.