Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Azungumza na Balozi wa Tanzania Nchini Uturuki Balozi Iddi Seif Bakari

 

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Tanzania Nchini Uturuki Mhe. Iddi Seif Bakari, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na  mgeni wake Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Uturuki Mhe.Iddi Seif Bakari (kulia kwa Rais) alipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo na kuja kumuaga akielekea katika Kituo chake cha Kazi Nchini Uturuki, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika mazungumzo na mgeni wake Balozi wa Tanzania Nchini Uturuki Mhe. Iddi Seif Bakari, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo Ikulu Zanzibar, alipozungumza na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Iddi Seif Bakari aliefika kwaajili ya kumuaga.

Alisema, Urutuki ni taifa lililoendelea kiuchumi ikiwemo sekta viwanda na kuimarika miundombinu yake, hivyo alimtaka Balozi huyo kuisimamia vyema sera ya Dilopomasia ya uchumi kwa kuangalia fursa ya uwekezaji wa viwanda kuja nchini kuwekeza badala ya kutegemeza zaidi bidhaa kutoka huko.

Aidha, alimtaka Balozi huyo kuwashajihisha wafanyabiashara wa Uturuki kuja Tanzania ikiwemo Zanzibar kufungua viwanda vya uzalishaji wa bidhaa zinazopendwa zaidi na Watanzania wengi.

Akizungumzia sekta ya utalii, Rais Dk. Mwinyi alimtaka Balozi Seif kuweka mkazo zaidi kwa kulishajihisha shirika la ndege la Uturuki linalofanya safari zake za moja kwa moja nchini, kuutangaza Utalii wa fukwe, Mji Mkongwe pamoja na mbuga za wanyama zilizopo nchini kwa kuwa na matangazo mengi ya utalii kwenye ndege za shirika hilo.

Dk. Mwinyi pia alimshauri Balozi Iddi Bakari kuwavutia wawekezaji wa miundombinu ikiwemo bandari, barabara na viwanja vya ndege ili kuimarisha maendeleo ya sekta hizo.

Kwa upande wake, Balozi Iddi Bakari alimuahidi Dk. Mwinyi na Watanzania kwa ujumla kuzitumia vyema fursa za uchumi ziliopo Uturuki kwa kuzipatia soko bidhaa za Tanzania likiwemo zao la pamba ambapo Uturuki ina mahitaji makubwa ya malighafi ya pamba kwa viwanda vya uzalishaji nguo nchini humo.

Mbali na kuahidi kuutangaza vyema utalii wa nchini, Balozi Bakari aliahidi kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania TTB pamoja na Kamisheni ya Utalii ya Zanzibar kutoa matangazo mengi kwa Shirika la ndege la Uturuki pamoja na kuimarisha uhusiano wa diplomasia nchini humo kuleta watalii wengi zaidi.

Sambamba na hilo, pia alieleza mikakakti ya kuimarisha ushirikiano na Uturuki kwa kuangalia uwezekano wa ndege ya mizigo ya ATCL kufanya safari zake nchini humo kwa kuboresha uhusiano wa biashara kwenye sekta ya usafirishaji wa mizigo na vifurushi baina ya Tanzania na Uturuki.

Balozi Iddi Seif Bakari aliteuliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa balozi wa Tanzania nchini Uturuki Aprili 05 mwaka huu, kabla ya uteuzi huo alikuwa, Konseli Mkuu nchini Dubai.

IDARA YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.