Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu
wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi akiongoza Kikao cha Tatu cha Kamati ya
Maandalizi ya mkutano wa 28 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mabadiliko
ya Tabianchi (COP 28) utakaofanyika Dubai kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 12,
2023. Kikao hicho kimefanyika Dodoma Oktoba 4,2023.
Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi amesema Mkutano wa 28 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28) utakaofanyika Dubai kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 12, 2023 ni fursa kubwa kwa Tanzania katika ushiriki wake.
Amesema hayo wakati
akiongoza Kikao cha Tatu cha Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa COP 28 Dodoma
Oktoba 4,2023 akisisitiza kuwa taasisi na sekta mbalimbali lazima ziungane
katika hilo.
Mitawi amesema kama
nchi lazima kwenda kimkakati ili kuonesha utayari wa kushirikiana na ulimwengu
katika mambo mbalimbali na kuonesha fursa zilizopo hapa nchini katika
uwekezaji.
“Bado hatujachelewa
sababu hii ‘COP’ sio ya mazingira pekee kama wengi wanavyodhani bali inagusa
sehemu kubwa katika taifa letu maana hapo ndio sehemu unaweza kupata kampuni
kubwakubwa za kuwekeza, unajifunza kutoka kwa wengine vitu vingi kwa wakati
mmoja kama vile usafirishaji, utalii, madini na ulinzi,” amesema Mitawi.
Kwa upande wake Mshauri
wa Rais, Masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi na Mazingira Dkt. Richard Muyungi amesema
Wizara ya Madini nayo inapaswa kushiriki katika hilo sababu hii ndio nafasi
kwao kujifunza kwa wenzao namna wanavyofanya na kupiga hatua katika eneo hilo
sambamba na Utalii, Wizara ya Kilimo na Wizara ya Maji.
“Kila mtu aone anao wajibu
kwenye hili ili kuhakikisha ushiriki wetu unakwenda kuzaa matunda huko
tunakokwenda kama taifa lakini kila mmoja akitazama upande wake namna ya
kuboresha hapa alipo kwa kujitangaza na kujifunza kwa wenzetu.”
Naye Mhandisi
Dorisia Mulashani kutoka Wizara ya Maji amesema watatumia fursa hiyo
kuhakikisha wanaboresha zaidi eneo la uwekezaji katika miradi ya maji ili
kukuza uchumi kwa kuwepo kwa mabwawa, umwagiliaji endelevu, kuboresha usafi wa
mazingira na uwezeshaji wa kijamii.
Mkutano huu
unatarajiwa kufanyika katika eneo la Blue
Zone (Expo City Dubai) na jumla ya washiriki takriban 100 kutoka
Tanzania Bara na Zanzibar wanatarajiwa kushiriki.
Matarajio ya COP 28
ni pamoja na kuhakikisha msimamo wa Tanzania unakubaliwa, kupata fursa za
upatikanaji wa rasilimali fedha kuwezesha utekelezaji wa miradi pamoja na
teknolojia za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Pia, nchi inatarajia kuongeza uwekezaji katika Biashara ya Kaboni, kutangaza jitihada za nchi na kuongeza ushiriki wa sekta binafsi katika jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Wajumbe wakiwa kwenye Kikao cha Tatu cha
Kamati ya Maandalizi ya mkutano wa 28 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa
Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28) utakaofanyika Dubai kuanzia Novemba 30 hadi
Desemba 12, 2023. Kikao hicho kimefanyika Dodoma Oktoba 4, 2023.
Wajumbe wakiwa kwenye Kikao cha Tatu cha Kamati ya Maandalizi ya mkutano wa 28 wa nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mabadiliko ya Tabianchi (COP 28) utakaofanyika Dubai kuanzia Novemba 30 hadi Desemba 12, 2023. Kikao hicho kimefanyika Dodoma Oktoba 4, 2023.
No comments:
Post a Comment