Habari za Punde

ZHSF na Pharm Access Wasaini Makubaliano ya Ushirikiano wa Kiutendaji

Kaimu Mkurugenzi mfuko wa  huduma za Afya Zanzibar  ZHSF (kushoto)  Yaasin Ameir Juma  na Mkurugenzi mkaazi Pharm Access Heri Marwa wakitia saini  hati za makubaliano ya ushirikiano wa kiutendaji  baina yao  huko Ofisi za mfuko ZHSF Michenzani mall mjini Unguja.

Na Rahma Khamis  Malezo Zanzibar. 

Mfuko wa huduma za afya Zanzibar wametiliana saini na Taasisi ya Pharm -Acess makubaliano ya ushirikiano ili kuimarisha utendaji kazi katika mfuko huo.

 

Akizungumza katika  hafla  hiyo iliyofanyika  Ofisi za ZSHF Michenzani Mall Kaimu Mkurugenzi Mkuu  Yaasin Ameir Juma amesema makuibaliano hayo yatasaidia kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wote.

 

Amesema  makubaliano hayo ni pamoja na  kushirikiana katika kusajili sekta isiyo rasmi na kuhakikisha upatikananji wa rasilimali za kutosha na kushirikiana katika  maeneo ya kitaamu  ili kuimarisha mfuko huo na kuendelea kutoa huduma bora kwa wazanzibar .

 

“mashirikiano kati yatu na taasisi ya Pharm -Acess ni ya muda mrefu kuanzia  kuusarifu mfuko huu  hadi kufikia hapa tulipo hivyo tunaendelea kushirikiana nasi ili kuendeleza utoaji wa huduma bora za afya kwa jamii” alifahamisha Kaimu Yaasin.”

 

Akigusia suala la kuendelea na usajili wa makundi mengine  Kaimu Mkurugenzi amesema  hivi karibumi wanatarajia kuanza usajili wa wanachama wa sekta binafsi ambapo Pharm-Acess  wamekuja kuunga mkono ili usajili huo uweze kukamilika kwa haraka.

 

Nae Mkurugenzi Mkaazi wa Taasisi ya Pharm-Acess  Heri Marwa amefahamisha kuwa  ushirikiano uliopo kati yao ndio umesaidia  uwepo wa mfuko huo na kuwaomba wananchi kuutumia mfuko ipaswavyo ili kupata huduma bora na za uhakika.

 

Aidha ameongeza kuwa  Taasisi hiyo imekuwa ikifanya  kazi na sekta mbalimbali za Serikali ikiwemo  afya ili  kuhakikisha wanafikia malengo  waliyojiwekea.

 

Hata hivyo Mkurugenzi Marwa  amesema watahakikisha kuwa watu ambao hawana uwezo na wanaishi katika mazingira magumu wanapata  huduma kupitia mfuko huo  ili kuboresha afya zao.

 

Itakumbukwa kwamba Mfuko wa Huduma za Afya Zanzibar umeanza usajili wa wananchama wake kupitia Sekta rasmi na kusema kuwa usajili wa sekta zisizo rasmi na makundi maalum utanza mara baada ya kukamilika kwa usajili wa sekta rasmi.



Mkurugenzi mkaazi Pharm Access Heri Marwa akizungumza na watendaji wa ZHSF mara baada ya kutiliana saini hati za makubaliano ya ushirikiano wa kiutendaji huko Ofisi za mfuko wa huduma za Afya Michenzani mall mjini Unguja.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.