Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud
Othman (kulia), wakizungunza pamoja na mfanyabiashara wa majimbi Shekh . Omar
Hamad huko katika soko la Mwanakwerekwe C wakati Mhe. Makamu alipokuwa kwenye
ziara ya kutembelea masoko m bali mbali ya mkoa wa mjini Magharibi laeo tarehe
28.03.2024. Picha na ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman masoud Othman
akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Mjini Mhe. Rashid Simai Msaraka wakati mhe.
Makamu akiingia katika viwanja vya soko la Kibandamaiti mkoa wa mjini Mgharib katika ziara yake
aliyoifanya leo tarehe 28.3.2024 kuangalia bei za bidhaa mbali mbali na upatikanaji
wake. Picha na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud
amewataka watendaji katika masoko mbali kujitahidi kuweka mazinira ya usafii katika
maeneo yote ya bisara tofauti ili kuepusha madhara ya afya za wananchi yanayoweza kupatikana kutokana na kutumia
vyakula vinavyouzwa katika hali ya uchafu unaoweza kuepukika.
Mhe. Othman ameyasema hayo mara baada ya kukamilisha ziara ya
kuyatembelea masoko mbali mbali katika mkoa wa mjini magharib kuona hali halisi
ya upatikanaji wa bidhaa pamoja na bei
zake hasa katika kipindi hiki cha mfungo wa
mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Amefahamisha kwamba masoko mengi katika mkoa huo wa mjini
Marib yanayouzwa bidhaa za nafaka , matunda, samaki pamoja na nyama na mboga
mboga yanakabiliwa na hali ya uchafu ikiwemo maji yanayotirika na kusababisha hali ya unyevu nyevu huku wafanyabiashara wakiendelea na shunguli zao katika hali hiyo jambo ambalo ni hatari
kwa afya ya mtumiaji.
Amefahamisha kwamba hali hiyo ni jambo linalohitaji kuzingatiwa
katika kuhakikisha kwamba kunawekwa na kudumishwa usafi wa mazingira katika
maeneo yote yanayoendelea na shughuli za biashara za aina zote angalau kwa kumwaga
kokoto ili kupunuza athari zinazoweza kusababishwa na hali ya uchafu.
Akizungunzia bei za bidhaa mbali mbali Mhe. Othman amesema
kwamba bidhaa nyingi bei ziko juu ikilinganishwa na hali halisi ya kipato cha
wananchi jambo ambalo linasababishia wananchi kuendelea kukubwa na ukali wa maisha.
Hata hivyo, amesema kwamba licha ya hali ya bei kuwa juu
lakini bidhaa nyingi za mahitaji ya wananchi hasa katika kipindi hiki cha
mfungo wa ramadhani zinapatikana kwa wingi katika masoko yote nchini.
Mapema baadhi ya wafanyabiashara hasa wa kitoweo cha nyama
walimueleza mhe. Makamu kwamba bei ya bidhaa hizo zimepanda kwa kuwa ngombe
wengi na mbuzi hulazimika kuaizwa kutoka Tanzania bara kwa vile Zanzibar haina
mifugo ya kutosheleza mahitaji ya
soko la walaji huku kukiwa kumepanda ushuru na ada mbali mbali za
kuiniza mifugo hiyo apa Zanzibar.
Aidha wamemuomba mhe. Kwamba serikali izinatie sana hali ya
upatikanaji wa mikopo ili waweze kuwa na ustawi imara wa kuendesha suuli zao za
biashara katika masoko na kwa bidhaa
mbali mbali jambo lityakalowasaidia kumudu kupambana vyema na hali ya maisha.
Pia wafanya biashara hao wa meomba serikali kuangalia ya bei
ya ukodishwaji wa Milango na wote kurejeswa katika seemu zao za biashara baada
ya ujezi wa ujenzi wa masoko mbali mbali unaoendelea kukamilika hasa kwa kuzingatia kwamba wengi wao
wamepoteza mitaji yao ya biashara kutokana na
hali ya biashara kuwa ngumu.
Mapema Mhe. Alitembelea soko la Mwanakwerekwe C, Soko la
Mwanakwerekwe raound abaut , soko la Kibanda Maiti pamoja na soko kuu la
darajani kuona hali halisi ya bei mbali mbali za bidhaa na upatikanaji wake
hasa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa ramadhani .
Imetolewa na ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo cake cha habari leo Alkhamis Maci 28, 2024..
No comments:
Post a Comment