Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Atembelea Soko la Machinga Tabora

Makamu  wa Kwanza wa Rais  wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman amesema kwamba kuwepo miundombinu imara na sahihi katika shughuli zozote za kibiashara ni jambo la lalazima ili kuwezesha shughuli hizo kufanyika vyema na kuleta tija kubwa kwa serikali na wafanyabiasara husika.

Mhe. Othman ambaye pia ni Mwenyikiti wa Taifa wa Chama  cha ACT wazalendo ameyasema hayo huko katika  soko la Machinga mjini Tabora i alipotembelea soko la wafanyabiashara hoa na kusikiliza kero mbali mbali walizonazo baada ya kuwatembelea.

Amefaamisha kwamba ni jukumu la mamlaka zinazohusika na kusimamia shughuli za biashara  kuaakikisha kwamba  wanteneneza mazingira wezeshi ya kibiashara ili kuweza kuwavuta wateja wa biasara sambamba na kulinda usalama wa mtumiaji.

Amesema kwamba serikali inawajibu wa kutayuarisa sera na mipano bora kwa kuwawezesa wafanyabiasara ndoo ndoo kujiajiri na kuhakikisha kwamba inakuwepo misingi  bora na imara ili waweze kuenesa kazi zao katika maeneo salama  hasa kwenye biashara za vyakula ambazo zinaahitaji usafi na unadhifu mkubwa ili kulinda pia afya ya mlaji.

Mapema wafanyabiashara wadogo wadogo wa  soko hilo maarufu la wamachinga  la mjini Tabora walimueleza Mhe. Ohtman kwamba soko hilo limejengwa kwa kuondosha njiani na kusababisha wafanyabiashara hao kutokukua na mazingira na mahali sahihi  pa kufanyia biashara kwa muda mrefu sasa .

Wamedai kwamba ali iyo imewafanya kukata mitaji yao ya biasara uku wakuendendelea kuwa na madeni ya benki kwa kusindwa kulipa kutokana na mitaji iyo kukosa faida na kufa kabisa kulikosababiswa na kokosa wateja kwa vile soko ilo alina mazinira rsafiki ya kuwavuta wateja.

Walimuomba Mhe. Othmani kuwapelekea kilio chao kwa Rais wa Jamuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan cha kukosa sehemu ya biashara   huku baadhi yao wakishindwa kulipa mikopo ya Benki waliyokopa kuendesha biashara hizo.

Wamesema kwamba viongozi mbali mbali wa nazi tofauti wamewai kufika na kupokea kilio chao lakini ati sasa hakuna  mabadiliko yoyote yaliweza kufanywa na serikali ya krekebisa mazingira hayo .

Wameiomba serikali kutenga  bajeti na kufanya jitiada za kulijena soko hilo kwendana na mazinira bora ya biasara na serikali iweze kukusanya kodi zitokanazo na ada na ushuru wa aina mbali mbali kutoka kwa wafanyabiashara wa hapo.

Katika atua nyengine  Mhe. Othman , alizindua mashina,  matawi,  na ofisi za Jimbo la ACT la Jimbo la Tabora mjini ambapo aliwataka kukiuna mkono chama  hicho  ili kuendeleza jitiada za kuzitumia rasilimali mbali mbali za ndani katika kukuza uchumi na kuondosha umasikini kwa wananchi.

Amesema kwamba Chama hicho  kimejipana kufanya mageuzi ya kiucumi na kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzania na kuwataka kukiunga mkono kwa kuhakikisha wanawachugua viongozi kutoka chama hico wa serikali za vijiji na mitaa katika uchaguzi wa baadae mwaka huu.

Mhe. Othman amemaliza ziara yake katika mkoa Tabora aliwasili mkoani Kahama kuendelea na ziara yake katika Mkoa wa Shinyanga anatarajiwa kumaliza ziara yake katika Mkoa kabla ya kurejea Zanzibar mwishoni mwa wiki hii.

Mwisho

Imetolewa na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha habari leo Jumatano tarehe 08.05.04. 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.