Habari za Punde

Katibu Mkuu Fatma Hamad Aipongeza Benki ya NMB kwa Kuiunga Mkono Serikali Katika Shughuli za Maendeleo Ikiwemo Michezo.

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB akimkabidhi  Hundi ya Tshs Milioni 50  Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu ikiwa ni udhamini wa  Kombe la  Mapinduzi  hafla iliyofanyika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,Migombani .

Kaimu Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB. Ahmed Nassour akimkabidhi Track Suit 100 Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu ikiwa ni mchango wa kudhamini siku ya Mazoezi Kitaifa  yatayofanyika kisiwani Pemba   hafla iliyofanyika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Migombani .

Kaimu Mtendaji wa Benki ya NMB Ahmed Nassour akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa makabidhiano ya Track Suit na Hundi ya Tshs Milioni 50 kwa Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu (hayupo pichani) katika hafla iliyofanyika Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Migombani  .
Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu akizungumza na waandishi wa habari wakati wa makabidhiano ya Track Suit na Hundi ya Tshs Milioni 50 iliyotolewa na Benki ya NMB ikiwa mchango wao wa kudhamini matembezi na mazoezi ya viungo pamoja na Kombe la Mapinduzi hafla iliyofanyika Wizara ya Habari Vijana Utamaduni na Michezo Migombani .
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu wakati wa makabidhiano ya hundi ya Tshs Millioni 50 na track sout iliyotolewa na Benki YA NMB hafla iliyofanyika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Migombani .

Katibu Mkuu, Wizara wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Ndg Fatma Hamad Rajabu ameipongeza Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika shughuli za maendeleo ikiwemo michezo.

Ameyasema hayo wakati wa Makabidhiano ya Track Suit na Hundi ya Tshs Milioni 50 iliyotolewa na Benki ya NMB ikiwa ni mchango wa kudhamini siku ya mazoezi Kitaifa na Kombe la Mapinduzi hafla iliyofanyika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Migombani.

 

Amesema mchango huo utasaidia mustakbali mzima wa michezo pamoja na kutoa hamasa kwa wachezaji katika mashindano ya Kombe la Mapinduzi ambayo yanatarajiwa kuanza January 03 .2025 .

 

Aidha amesema katika mashindano hayo Timu ya Kimataifa zinazoshiriki mashindano ya Chan zitakuwepo  pamoja na wazawa wa Zanzibar Herous  .

 

Katibu huyo amempongeza Waziri wa Habari Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita kwa kazi kubwa anayoifanya kuisimamia na kuiongoza Wizara hiyo.

 

Nae Kaimu Mtendaji wa Benki ya NMB  Kanda ya Zanzibar Ahmed Nassour amesema mchango wa track suit 100 utasaidia kuhamasisha mazoezi pamoja na kutoa hamasa katika siku ya mazoezi kitaifa ili kufanikisha shamrashamra ya Maadhimisho ya miaka 61 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 

Amesema NMB ni miongoni mwa wadau wakubwa katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  

 

Amefahamisha kuwa Benki hiyo itaendelea kutoa mashirikiano kwa Serikali ili kuhakikisha unaimarisha mustakbali ya michezo na afya kwa Wazanzibar.  

 

Ameeleza kwamba katika miaka 12 mfululizo Benki ya NMB inaunga mkono Serikali katika kudhamini michezo jambo ambalo linaonyesha kuwajali wananchi wao.

 

 Imetolewa na Kitengo cha Habari Mawasiliano na Uhusiano.

 

WHVUM.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.