Habari za Punde

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Ameweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Bweni la Wanaume Chuo Cha UVCCM Zanzibar

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiondoa pazia kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Mabweni ya Wanafunzi Wanaume wa Chuo cha Vijana wa UVCCM Wilaya ya Kati Unguja, akiwa na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndg.Mohamed Ali Kawada, hafka hiyo iliyofanyika leo 17-2-2025
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akitembelea mabweni ya Wanafunzi wa Chuo cha Vijana wa UVCCM akipata maelezo kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Zanzibar Ndg.Abdi Mahmoud Abdi (kushoto kwa Rais)  baada ya kuweka Jiwe la Msingi la ujenzi huo leo 17-2-2025, katika Wilaya ya Kati Unguja na (kulia kwa Rais) Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mohamed Ali Kawaida na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Vijana wa UVCCM, wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Mabweni ya Vijana Wanaume wa Chuo cha UVCCM Zanzibar , Wilaya ya Kati Unguja leo 17-2-2025

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dkt,Hussein Ali Mwinyi amesema Chama cha Mapinduzi [CCM] kinaandaa Mpango Mkakati Maalum kuhakikisha Jumuiya za Chama hicho zinakuwa na nguvu ya kujitegemea na Miradi Mikubwa ya Maendeleo. 

Dkt,Mwinyi ambae pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ametoa tamko hilo alipozungumza baada ya kuweka jiwe la msingi la Bweni la Vijana wa Kiume wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi [UVCCM].

Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa ni lazima Chama nacho kiache alama ya uongozi itakayokumbukwa kwa muda mrefu kwa kufanya mambo makubwa ya maendeleo na miradi ya Chama katika ngazi zote.

Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM Zanzibar amefahamisha kuwa Alama iliyoachwa na Serikali katika Sekta zote za Maendeleo ni lazima pia iachwe ndani ya CCM.

Dkt,ameipongeza UVCCM kwa kufanikiwa kujenga Jengo hilo litakalotumika kwa harakati mbalimbali za Jumuiya hiyo.

Aidha amesema Chama Cha Mapinduzi kitaendelea kuunga Mkono juhudi za Jumuiya hiyo kwa hali na Mali ili dhamira ya kuwajenga vijana kuwa wazalendo na kuwapatia mafunzo mbalimbali ifanikiwe.

Dkt,Mwinyi ameisisitiza UVCCM kuendeleza kasi ya uhamasishaji uandikishaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura na kuhakikisha vijana wengi wanajiandikisha litakapoanza kwa upande wa Unguja hivi karibuni. 

Ametoa wito kwa vijana kutobaki nyuma siku ya kupiga kura ili CCM ipate ushindi wa kihistoria na kuendelea kushika Dola. 

Naye Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM Taifa,Mohammed Ali Kawaida amesema Kauli ya Mitano Tena ni kwa ajili ya viongozi wawili tu ndani ya CCM ambao ni Mwenyekiti wa CCM Taifa,Ndugu Samia Suluhu Hassan na Makamu wa Mwenyekiti CCM Zanzibar, Ndugu Hussein Ali Mwinyi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.