Habari za Punde

Kikwete: Serikali Kusaini Muongozo Wa Kima Cha Chini Cha Mshahara Kwa Sekta Binafsi.

 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira,Vijana na Wenye Ulemavu Mhe.Ridhiwani Kikwete akikata utepe kilifungua jengo la Ofisi la Biashara la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) Jijini Arusha. 
SERIKALI imesema hivi karibuni inatarajia kusaini kuwa Sheria miongozo wa kima cha chini cha mshahara kwa Taasisi binafsi zinazofanywa kazi nchini.

Amesema katika muongozo huo unatarajia kuainisha viwango vipya vya mshahara ambapo wafanyakazi wa sekta binafsi watakuwa wanalipwa.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira  Vijana na Wenye Ulemavu Mhe.Ridhiwan Kikwete amesema hayo jijini Arusha katika uzinduzi wa jengo la  biashara Shirikisho La Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) lililoko mkabala na soko kuu.

Kuhusu muongozo huo amesema mazungumzo yameshafanyika baina ya wadau ambao ni Taasisi binafsi na wasimamizi wa sera lakini pia uongozi wa timu ya Wizara iliyopewa jukumu la kusimamia marekebisho hayo.

Amesema kikao kilichobakia ni cha mashauri ambapo watashauriana na wenzao juu ya viwango vilivyowekwa na baada ya hapo mapema mwezi ujao huenda wakasaini marekebisho hayo.

“Hivyo nawaambia Wafanyakazi kuwa Rais Dkt Samia anathamini sana maslahi yenu,” amesema Ridhiwan na kuongeza kuwa serikali itaendelea kuboresha sheria za Wafanyakazi ili ziendane na mahitaji ya wafanyakazi.

Amesema  Serikali  itaendelea kushirikiana na Wafanyakazi  bega kwa bega katika:Kutekeleza mikakati ya kuongeza ajira;Kulinda haki za wafanyakazi;Kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya mazungumzo.







No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.