WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa
Umma na Utawala Bora Haji Omar Kheir, ameliambia Baraza la Wawakilishi kuwa
wananchi wengi wa Zanzibar
bado hawajui misingi mikuu ya inayojenga utawala bora.
Waziri huyo aliyasema hayo jana wakati
akijibu suala la Mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe, Ismail Jussa Ladhu,
aliyetaka kujua matokeo ya utafiti juu ya utawala bora uliofanywa na wizara
hiyo kwa kushirikiana na International Law and Policy Institute.
Akijibu suala hilo waziri huyo alisema tayari ripoti hiyo
inafanyiwa kazi, lakini katika hatua za awali zimeonesha bado Wazanzibari
hawaijui misingi mikuu inayojenga utawala bora.
Alisema katika utafiti huo pia iligundua
wananchi wengi wanajua vyema maana ya rushwa na madhara yake na matokeo ya
utafiti huo yanatarajiwa kuwekwa hadharani mara baada ya kukamilika hatua za
upokeaji wa ripoti hiyo kutoka kwa watafiti.
Alisema kuchelewa kutolewa hadharanai kwa
ripoti hiyo kunatokana na kubainika kuwapo kwa makoseo ndani ya ripoti hiyo
baada ya Makatibu wakuu kuipitia na kubaini kuwapo kwa matatizo ya aina hiyo.
Alisema kazi hiyo baada ya kukamilika
serikali inafikiria kuigawa ripoti hiyo kwa wananchi ikiwa ni hatua ya kuona
utafiti huo unawafikia wengi.
Waziri huyo alieleza kuwa serikali katika
kuhakikisha inalifanya hilo kwa kuzifanyia kazi
tafiti hizo kama ni taarifa za msingi kwa
mfumo wa mawasiliano kwa tafiti ambazo zitafanywa hapo baadae.
Alisema katika kuufanya utafiti huo wizara
hiyo iliwahoji makundi mbali mbali wakiwemo wananchi mbali mbali katika shehia
za visiwa vya Unguja na Pemba, Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi na Watumishi wa Umma ambapo mambo waliyoulizwa ni pamoja
na Utawala bora, rushwa na huduma za kijamii kwa umma.
Akijibu suala la nyongeza la Mwakilishi huyo
aliyetaka kujua ni kwanini ripoti hiyo iliwasilishwa kwa makatibu wakuu pekee,
alisema ilifikishwa huko kutokana na kuwa ndio utaratibu wa serikali kufikisha
ripoti hizo kwa kamati ya wataalamu na baada ya kujirisha inakusudia kufikishwa
mbele zaidi.
0 Comments