6/recent/ticker-posts

Zawadi ya krismasi: Nsami, Menina na Husna wa Epiq BSS waachia nyimbo zao mpya

Wadada wakali wa Epiq BSS waliofanikiwa kuingia TOP 10, Nsami Nkwabi, Husna Nassor na Menina Atik, wamewapa mashabiki wao zawadi ya nyimbo mpya kwa ajili ya sikukuu ya Christmass.
Wadada hao ambao walitoa burudani ya kutosha wakati wa mashindano hayo, hivyo kujijengea mashabiki kibao, Husna akiwa kajikita kwenye miziki ya Taarab, na Nsami na Menina wakiimba miziki laini, wamesema zawadi hiyo ni maalumu kwa mashabiki wao kwa ajili ya Christmass.
Nsami, ambaye alishika nafasi ya nne, wimbo wake unaitwa ‘NILIDHANI’, ambao kaufanyia studio ya Surround Sounds chini ya mtayarishaji EMA the Boy, na umendikwa na mkali kutoka THT, Amini.

Akiuzungumzia wimbo huo, Nsami anasema ameufanya wimbo huo mapema ili kuonyesha uwezo wake, na anaamini utawashika wapenda burudani nchini.
‘Wimbo huu unamuonyesha Nsami, ambaye wengi wenu mlipigia kura wakati wa mashindano, hivyo ninaomba muendelee kunisapoti kwa zangu nyingi zinazokuja’ anasema Nsami.
Kwa upande wake yule mshiriki aliyeingia kwa Wild Card, Menina, yeye wimbo wake unaitwa ‘DREAM TONIGHT’ , ambao ameufanya chini ya Studio ya Surround Sound, mtayarishaji akiwa EMA the Boy na mtunzi akiwa Nash Designer.
‘Dream tonight ni wimbo ambao hakika utawafanya watanzania wamjue Menina hasa, kwani ni wimbo ambao ni wa kiburudani zaidi tofauti na wengi walivyonizoea nikiwa katika Epiq BSS’ anasema Menina.
Mshiriki Husna, ambaye alijijengea jina kwa kuimba nyimbo za Taarab, ameendeleza ukali wake kwa kutoa kibao chake cha mduara, ‘NAWAMIMINA’ kikiwa kimetayarishwa na EMA the Boy na kuandikwa na Nash Designer.
‘Nimeamua kuendelea kuwapa burudani ambayo wengi wenu mliizoea toka kwenye mashindano ya BSS, lakini nina uhakika wimbo huu utaleta mabadiliko kwenye soko la muziki wa Taarab hapa nchini’ anasema Husna.
Nyimbo hizo zinatoka zikufuatia wimbo wa Wababa Mtuka, mshindi namba tatu wa Epiq BSS uliotoka wiki iliyopita unaoitwa, My Wife,ambao unafanya vizuri kwenye radio zote hapa nchini

Post a Comment

0 Comments