6/recent/ticker-posts

Adaiwa kuwa Mwizi wa Kuku Apata Kipigo.

Na Mwandishi Wetu Pemba.
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Sadiki Iddi Mbarouk, mkaazi wa limbani Wete amelazwa katika hospitali ya Wete baada ya kupata kipigo kutoka kwa Wananchi wenye hasira na kumsababishia majaraha na kulazwa katika hospitali hiyo kwa matibabu.

Kijana huyo anayekisiwa kuwa na umri wa miaka kati ya 25 na30 amefikwa na kadhi hiyo kutoka kwa wananchi wenye hasira akituhumiwa kukutwa na kuku wanaosadikiwa ni wa wizi.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa shida wakati akiendelea kupata matibabu katika hospitali ya Wete Sadiki amedai kuwa mkasa huo umempata jumatatu ya mei 19 mwaka huo majira ya saa nne asubuhi huko utaani wete.

Na kusema amepigwa na watu wengi tu,wanadai kwamba mimi nimeiba kuku asubuhi huko utaani na walionipiga wanajuwa wote kwani sikumbuku kuiba kitu cha mtu, alisema.

Nae Daktari wa zamu katika wodi ya wanaume alimwambia mwandishi kuwa wamepokea kajeruhi huyu majira ya saa nne na nusu asubuhi.

Alifahamisha kuwa kijana huyo amepata maumivu sehemu za kichwa ambazo amepigwa na kupasuka na katika sehemu ya mkono wake wa kulia ukiwa na maumivu yaliosababishwa na jaraha.

Alisema kuwa tayari majeruhi huyo amepatiwa huduma za mwanzo ikiwa na pamoja na kusonwa sehemu alizoumia na kupigwa picha ya X-RAY, ili kujuwa hali ya mkono wake.


Ni kweli tumepokea majeruhi mmoja anayefahamika kwa jina la Sadiki Said Mbarouk, huyu amefikishwa hapa akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la Polisi

Nae Kamanda wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Shekhan Mohammed Shekhan,amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wananchi kuacha kuchukuasheria mikononi mwao.

Alisema kuwa pamoja na falsafa ya Polisi Jamii kusaidia kukabiliana na vitendo viovu lakini vyema wananchi wazingatie ukamataji salama kwa kuhakikisha kwamba wahusika wanafikishwa kwenye vyombo vya dola salama.

Ninawaomba wananchi wazingatie suala la ukamataji salama na kuacha kujichukulia sheria mikononi mwao bali wawafikishe kwenye vyombo vya sheria wahalifu wanapowakamata,alisisitiza Kamanda.          


    

Post a Comment

0 Comments