Na Mwandishi Wetu.
Jumla ya shilingi bilioni
1,553,484,832.zimetolewa mikopo ipatayo 755 kwa wananchi 5,200 wa Unguja na Pemba
kwa lengo la kujiimarisha kiuchumi.
Mkurugenzi Idara ya Mikopo
Zanzibar Ndg. Suleiman Ali Haji, alisema hayo wakati akizungumza na mwandishi
Ofisini kwake Vuga mjini Unguja.
Alisema tangu kuazishwa kwa
mfuko huo wa Uwezezeshaji Wananchi Kiuchumi mwaka 1991 na mifuko ya AK na JK
mwaka 2009, hadi kufikia juni 30 mwaka
2013 umewanufaisha walengwa hao.
Jumla ya walionufaika moja
kwa moja na fedha hizo ni watu 5200 kupitia mikopo hiyo 755 iliokwishatolewa,
kwani baadhi ya mikopo imetolewa katika vikundi vya watu kuazia watano hadi 25
kupitia SACCOS.
Mkurugenzi huyo aliongeza
kuwa kati ya fedha zote ambazo zimetolewa katika mfuko wa JK na AK, 1,075,264,832. ambazo zimetolewa katika
wilaya sita za Unguja, ambazo shilingi 478,220,000 zimetolewa kwawilaya nne za
Pemba, hadi kufikia 30 juni 2013.
Akizungumza kwa upande wa
marejesho ya mikopo, Mkurugenzi alisema jumla ya shilingi milioni 967,881,671. ni miongoni mwa fedha hizo
zilizotolewa, zimeweza kurudishwa tangu mfuko huo ulipoazishwa hadi 30,juni
2013, kama inavyoonekana hapa chini.
Hata hivyo, alikiri kuwa kuna
baadhi ya wananchi hadi sasa hawajarejesha mikopo hiyo, jambo ambalo limeenda
kinyume na masharti husika ya mikopo hiyo.
Kwa kweli wanaturejesha nyuma
wale wote ambao hawakurejesha mikopo na kwamba ile dhana ya baadhi ya watu
wanaosema kuwa mikopo hiyo ya Serekali ni lazima iliwe basi wanaenda kinyume na
masharti yetu.
Aidha alisema kuwa mikopo
hiyo haina riba kwa sasa jambo ambalo pia linawapa fursa zaidi wananchi
kuchukua mikopo hiyo.
Sambamba na hilo
lakini Mkurugenzi alisema kuwa mikopo hiyo imewalenga sana wanawake 9,870 na wanaume 6,870
wamefaidika namikopo hiyo tangu kuazishwa mwaka 1991.
Tangu kuazishwa huduma ya
utoaji mikopo mwaka 1991 jumla ya shilingi bilioni 1,027,289,850. zimetolewa
ambapo fedha zilizorejeshwa hadi sasakufikia mwaka jana ni shilingi milioni
967,881,671.
Mifuko imewezeasha wananchi
hasa masikini wa mijini na vijiji kujipatia mitaji iliowawezesha kufanya
shughuli za kilimo, biashara, uvuvi na ufugaji,hivyo mikopo imekuwa chazo cha
upatikanaji wa ajira.
Aliwataka wananchi kuitumia
fursa ya mikopo ili kujiendesha kiuchumi na maendeleo yafamilia na taifa kwa
ujumla katikampango wa kupunguza umasikini nchini.
0 Comments