6/recent/ticker-posts

Wadau Wataka Waharibifu Mazingira Kubanwa.

Na Mwandishi Wetu. 
Kutokuwepo kwa sheria ya kuwabana  waharibifu wa mazingira ya misitu kunasababisha uharibifu kuongezeka nchini hapa.

Hayo yelielezwa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Uhifadhi Mazingira wa Kikundi cha Kumsa, Ndg Voti Mtumwa Mkadam, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii huko kiwengwa wilaya ya Kaskazini B Unguja.

Alisema hali hiyo ya uharibifu wa mazingira unasababisha ongezeko kubwa la uharibifu mazingira kwa kasi kubwa na kusababisha nchi kugeuka na kuwa jangwa.

Alifahamisha kuna baadhi ya vyombo vya sheria havitendi haki kwa vile wanakuwa wanawaachilia wananchi wanaoharibu misitu bila ya kuwapatia adhabu yoyote, jambo amnalo linatejesha nyuma juhudi za kuzuia uharibifu huo.

Alisema licha ya kuwepo kwa utoaji wa elimu ya utunzaji wa mazingira, lakini bado kuna wananchi kila kukicha wanaendelea kukata misitu hali ambayo inasababisha maporomoko ya ardhi pamoja na kupotea kwa rasilimali hizo.


Kila mmoja ana jukumun la kutunza mazingira na kuhakikisha kuwa ni mlizi wa nafasi yake na mlizi wa mweziwe yoyote atakayeonekana anafanya kitendo hicho cha uharibifu wa mazigira,hatua kali zichukuliwe juu yake na hakuna msamaha,alisema Mwenyekiti huyu kwa uchungu.

Mwenyekiti huyo alisema kwa sasa athari zimejitokeza kwa wingi ikiwa ni pamoja na bahari kuja juu kwa kasi sasa pamoja na ongezeko kubwa la joto,hivyo ni vyema kuwa tayari kukabiliana na athari hizo.


Aidha, alisema katika kuhakikisha uharibifu wa misitu unadhibitiwa ni vyema kuwa na ushirikiano madhubuti baina ya wananchi na jeshi la Polisi ilikuona kwamba uharibifu wa misitu unaondoka hapa nchini kwetu.               

Post a Comment

0 Comments