6/recent/ticker-posts

Wajumbe wa Baraza, Bunge wana Kinga Maalum SMZ.

Na Mwandishi Wetu
Serekali ya Mapinduzi Zanzibar imesema hakuna shria yoyote itakayoweza kuchukuliwa dhidi ya Mjumbe wa baraza la Wawakilishi kwa kuzungumza na kujadili mambo mbalimbali wakiwa ndani ya vikao vya baraza na Bunge.

Serekali imesema kila baraza au Mabunge yoyote duniani yanalindwa na kanuni zake hivyo mjumbe yoyote wa baraza anaweza kuzungumza ndani ya baraza maelezo yake yote aliyoyasema na hatafunguliwa mashtaka ya madai au jinai.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohammed Aboud  Mohammed, alipokuwa akijibu suali la Mwakilishi wa jimbo la Wawi Pemba Mhe. Saleh Nassor Juma, alietaka kujua Sheria ya Zanzibar  zinasemaje kwa Waheshimiwa wanaokwenda kinyume na kiapo walichoapa juu ya kuiteteaKatiba ya Zanzibar .

Waziri Aboud alisema sheria ya Baraza la Wawakilishi (kinga maalum na fursa) namba 4 ya mwaka 2007 kifungu cha tatu na kifungu cha nne kimeweka kinga kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuwa na uhuru wa kuzungumza na kujadili wakiwa ndani ya vikao vya baraza na uhuru huo hautohojiwa na mahakama yoyote au sehemu yoyote nje ya Baraza.


Awali katika suala la msingi la Mwakilishi huyo alitaka kujua Sheria za Zanzibar zinasemeja kwa Waheshimiwa wanaokwenda kinyume na kiapo walichoapa.

Mwakilishi huyo alifahamisha kuwa katika kutekeleza kazi zao Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walikula kiapo cha kulinda, kuituza na kuitetea Katiba ya Zanzibar lakini kuna baadhi yao wanakwenda kinyume na kiapo hicho.

Alisema kuna baadhi ya wajumbe wa baraza ambao pia ni wajumbe wa bungev la katiba wamethubutu kuikebehi Katiba ya Zanzibar na kuilinganisha na katiba  ya timu za mpira sambamba na kulinganisha na bendera za  Simba na Yanga pamoja na ile ya Uamsho.


Waziri Aboud akijibu suali la nyongeza la mwakilishi huyo, alisema ni vyema ikatumika lugha ya staha kwa viongozi  pamoja na nchi ili kulinda heshima ya baraza pamoja na viongozi wake.           

Post a Comment

0 Comments