6/recent/ticker-posts

Kutoka Baraza la Wawakilishi.

Na Maryam himid kidiko na Kijakazi Abdallah-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea na juhudi zake za kuwaelimisha Wananchi ili waachane na tabia ya kujenga karibu na  maeneo ya Kambi za Kijeshi kwa lengo la kuepuka usumbufu pamoja na madhara yanayoweza kuwakumba baadae.

Hayo yameelezwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa pili wa Rais Mohamed Abuod wakati akijibu suala la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Saleh Nassor Juma katika kikao cha tano kinachoendelea cha Baraza la Wawakilishi. 

Mhe.Saleh alitaka kujua kuwa lini Serikali itafikiria kuzihamisha kambi za kijeshi zilizopo karibu na Makaazi ya Raia na kuzipeleka nje ya Miji na Vijiji.
Waziri Aboud alifahamisha kuwa katika nchi yoyote ile duniani kambi za kijeshi huwekwa Kimkakati kwa lengo la kuimarisha ulinzi na usalama katika nchi husika ikiwemo Zanzibar.

Alisema Kambi zilizopo nchini sio tatizo na kwamba zimewekwa kwa kuzingatia haja ya kiulinzi, usalama na mazingira ya Zanzibar ilivyo.


Ameongeza kuwa Jeshi la Wananchi linahitaji maeneo maalum yakiwemo ya kufanyia mazoezi ili kujiweka tayari kwa adui yoyote Yule atakaeingia katika nchi kwa kufanya uadui.

Hata hivyo aliongeza kuwa kwa sasa kambi zilizopo zilijegwa kwa miaka mingi iliyopita na kwa wakati huo maeneo hayo hayakuwa karibu na makaazi ya raia.

Amesema kutokana na maeneo ya Kambi hizo kuvamiwa na Wananchi kwa lengo la kuanzisha Makaazi limekuwa tatizo na kwamba juhudi zinafanywa kuondokana na tatizo hilo ikiwemo kuwaelimisha Wananchi juu ya Madhara yanayoweza kujitokeza

Post a Comment

1 Comments

  1. Hoi lugha ya wananchi kuvamia maeneo ima ya kambi, kilimo au maji Mimi hunishangaza sana. Hivi tujiulize kwa Zanzibar hii kuna maeneo yaliyopimwa Maalim kwa makaazi ya wananchi? Hivi tulitarajia watu wajenge wapi wakati Serikali yenyewe haijatenga hayo maeneo yanastahiki kujengwa kwa ajili ya makaazi. Ikitokea maeneo Fulani yamepimwa basi wanaipewa night hao halo wakubwa ima makatibu wakuu, wabunge, makamishna name wanaofanana nao. Kwa style hoi tutapiga kelele kila siku eti wananchi wanavamia kum be sababu kuu ni serikali yenyewe

    ReplyDelete