6/recent/ticker-posts

Wananchi Rombo wachoma moto ofisi za kilimo

Na Kija Elias, Rombo
WANANCHI wa kijiji cha Aleni wilayani Rombo, mkoani Kilimanjaro, wamevamia jengo la ofisi ya idara ya kilimo na umwagiliaji na kisha kulichoma moto kupinga kuondolewa  kwa Mwenyekiti wa kijiji hicho kwenye jengo la Chama cha Mapinduzi na kuhamia kwenye jengo la idara hiyo.
Kuchomwa kwa jengo hilo kunafuatia kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, aliyoitoa hivi karibuni ya kupiga marufuku viongozi wa serikali za mitaa wanaoishi kwenye nyumba zinazomilikiwa na CCM.
Akizungumza na Zanzibar Leo, Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Rombo, Elinas Pallangyo, alisema tukio la kuchomwa moto kwa jengo hilo limetokea baada ya Mwenyekiti wa kijiji hicho  kuagizwa kuondoka kwenye jengo la CCM na kuhamia kwenye jengo la idara ya kilimo.
Alisema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia FebruarI 9 mwaka huu ambapo wananchi hao wanadai majengo ya CCM ni mali ya wananchi kwani yalijengwa kwa michago ya wananchi na si ya chama.

Alifafanua kuwa ofisi hiyo imeteketea pamoja na mali zote ambapo mpaka sasa thamani halisi haijajulikana na  jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi ili kuwabaini wahusika.

Post a Comment

0 Comments