6/recent/ticker-posts

Dk Shein, Aizundua Meli Mpya ya MV Mapinduzi II Zanzibar.

Meli Mpya ya MV MAPINDUZI ikiwa imefunga Gati ya Malindi wakati wa Uzinduzi wake uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwasili katika bandari ya Zanzibar akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe Abdalla Mwinyi Khamis.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwasili katika bandari ya Zanzibar akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwasili katika bandari ya Zanzibar akisalimiana na Viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, alipowasili katika eneo la bandari ya Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar Abdalla Juma,akitowa maelezo kwa Rais sehemu ya kukaa abiria wakisubiri kupanda katika Meli ikiwa katika eneo la Bandari ya Malindi Zanzibar 
Sehemu ya kupumzikia abiria wakisubiri kupanda Meli iliojengwa na Shirika la Bandari Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akiwa na Mkurugenzi wa Bandari na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano, wakitembea kuelekea sehemu ya Gati ya Malindi kwa ajili ya uzinduzi wa Meli Mpya ya Mv Mapinduzi 2.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Afisa Uhusiano wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano Nafisa Madai akitowa maelezo kwa Rais Dk Shein, kuhusiana na utengenezaji wa Meli hiyo wakati wakitiza TV. ikionesha jinsi ya utengenezaji wa Meli hiyo huko Nchini Korea ya Kusini. 













Sehemu ya VIP ina uwezo wa kuchukua abiri 55.
       Waheshimia wakiwa katika sehemu ya daraja la kwanza 
Mfanyakazi wa Meli ya Malipinduzi  II akiwa katika sehemu ya abiria daraja la kwanza 
Sehemu ya mgahawa kila sehemu ya abiria inajitegemea kwa mgahawa wake kwa kutoa huduma ya chakula kwa abiria
Sehemu ya kukaa Abiria wa daraja la Pili 
Sehemu ya maegesho ya magari yanayopakiwa kusafirishwa ina uwezo wa kuchukua magari 60
Chumba cha kuhifadhia maiti kikiwa katika meli hiyo na Kuna sehemu ya msikiti kwa ajili ya kusalia Abiria wakiwa safarini. 
Moja ya Boti za Kuokolea ikitokea Dharuwa wakati safari zake ikiwa na uwezo wa kuchukua abiria 66 kwa wakati mmoja 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akiteremka katika Meli ya Mv Mapinduzi  II baada ya kuizindua na kuitembelea Meli hiyo ya Mpya na ya Kisasa kujionea vitu mbalimbali vilioko katika Meli hiyo. 

Post a Comment

0 Comments