6/recent/ticker-posts

Wahitimu 145 mafunzo ya afya wapokea vyeti SUZA




Na Mwandishi Wetu, SUZA
Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar   (SUZA) kimewatunuku vyeti  wahitimu 145 wa mafunzo  ya wahudumu wa afya ya ngazi  ya jamii  (CHW) yaliyowajengea uwezo wa kutoa huduma bora kwa jamii.
 Mafunzo hayo ya miezi sita  yamewashirikisha wanawake 131 na wanaume 14  ambao wamejifunza kutoa huduma kwa uweledi zaidi kama vile kupima sukari, maradhi ya moyo, huduma za lishe za watoto na kukusanya takwimu.
Akizungumza kwa niaba ya Kaimu Makamu Mkuu wa SUZA, Prof. Abdi Talib Abdalla,   Kaimu Mkuu wa Skuli ya Afya na Sayansi za Tiba-SUZA  Dk. Ali Adnan  Idarous, aliwahimiza wahitimu hao kufuata miongozo waliyojifunza ya utoaji huduma bora bila ubaguzi wa aina yoyote.
Katika mahafali yaliyofanyika viwanja vya Skuli ya Afya iliyoko  Mbweni tarehe 7/02/2026, Prof. Abdallah  aliwakumbusha  wahitimu hao  wanapokwenda kufanya  kazi kwenye jamii watalazimika kufuata miongozo kama walivyoelekezwa kwenye mafunzo waliyoyapata, kuibua changamoto na kuzifanyia kazi sambambana  na kuwasaidia wananchi  kwa moyo wao wote.

Vile vile, walijifunza namna ya kujikinga na maradhi ya kuambukiza na pia kutunza siri za wagonjwa. Mafunzo hayo ni endelevu na yanaendelea kwa wanafunzi wengine wapya 100. 

 

Post a Comment

0 Comments