6/recent/ticker-posts

Serikali kuimarisha Viwanja vya Michezo


 Mkoa wa Mjini Magharibi. 17/01/2026.


Waziri wa Habari, Sanaa Utamaduni na Michezo  Mhe, Dk. Riziki Pembe Juma amesema  Serikali  itaendelea kuimarisha Viwanja vya Michezo ili  kuongeza hamasa ya Wananchi.

Ameyasema hayo wakati wa  ugawaji wa Zawadi kwa Washindi  wa mbio za Baskeli, zilizoanzia Mapinduzi Square Kisonge na kumalizia Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi B.

Amesema Ujenzi na uimarishaji wa Miundombinu ya Michezo Nchini, imesaidia kuongeza shauku kwa Wananchi sambamba na kujenga Afya zao kiakili na kimwili.

Aidha Dkt. Riziki ameahidi kuwa Serikalii itaendelea kuwaenua Wanamichezo kupitia makundi yao, ikiwemo Michezo ya Asili kama vile Baskeli, Bao na Karata.

Nae Mkurugenzi wa ABM. Foundation  Abdallah Idrissa Majura  amesema lengo la kuandaa mashindano hayo ni kuendeleza Uridhi wa Mzanzibar ili usipotee.

Aidha Majura, ameiomba Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kuweka siku maalum ya mbio za Baiskeli sambamba na kuomba kuwasaidia kupata Ufadhili.

Kwa Upande wake Katibu  wa Chama Cha Baskeli Zanzibar (CHABAZA) Saleh Kijiba Said ameipongeza Serikali kwa kuimarisha Miundombinu ya Barabara jambo ambalo limeondosha usumbufu wakati wa Mashindano na mazoezi.

Mashindano hayo, yamedhaminiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Nyumba Tanzania  (NHC) na Mamlaka ya Ngorongoro (MCAA) ambapo jumla ya Wapanda Baiskeli 30 walioshiriki na kupatiwa zawaidi ya  Fedha taslim.

Imetolewa na Kitengo cha Habari,

WHSUM

Post a Comment

0 Comments