6/recent/ticker-posts

Kutembelea wagonjwa ni fursa ya kuelewa shida za wananchi - OMO





 

Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba ziara za kuwatembelea wagonjwa na wenye shida katika kipindi cha mwezi mtufufu wa ramadhani ni fursa muhimu kwa viongozi kutambua kwamba wanadhamana kubwa kwa wananchi kuzielewa shida na matatizo waliyonayo na kutafuta namna sahihi ya kuyakabili.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko Milimani Kiembe Samaki wilya ya Magharib B alipofanya majumuisho baada ya kukamilisha ziara ya kutembelea wagonjwa ndani ya Wilaya ya Magharib A na B akiwa katika siku ya tatu ya mfululizo wa ziara zake za aina hiyo katika kisiwa cha Unguja.

Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mstaafu, amesema kwamba wananchi wanayo matatizo na shida nyingi ambapo kupitia ziara kama hizo viongozi wataweza kuzitambua kwa urahisi kwa kufika mwenyewe kwenye maeneo yao wanayoishi wananchi.

Amesema  ndani ya kipindi cha miaka mitano yakuendeleza ziara hizo amepata uzoefu mkubwa pamoja na kujifunza mambo mengi kutoka kwa wananchi wenyewe na kuwaomba viongozi wa ngazi mbali mbali kuendeleza jambo hilo lenye faida kubwa kwa wananchi.

Mhe. Otman amesema njia pekee ya kuyaelewa vyema matatizo ya wananchi  ni  kuyaona na kwamba ziara hizo pia zimempa uzoefu mkubwa kwa kuyajua vyema  matatizo mengi ya wananchi ambayo awali kabla ya ziara hizo kama kiongozi hakuweza kuyatambua.

Hivyo, amewapongeza viongozi mbali mbali  waliosaidia kuandaa na kufanikisha ziara hiyo na kusisitiza kwamba ada hiyo iliyoachwa na wazee waliondangulia ni vyema kuendelezwa ili kuwasaidia wananchi hasa wenye hali ngumu  ambayo mwaka huu pia mechangviwa  na kuwepo uhaba wa mvua.

Mapema mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Magharib B kichama  Ali Juma, amemshukuru na kumpongeza mhe. Othman kwa kukubali kuendeleza ziara hizo kama zilivyokuwa zikifanywa na watangulizi wake.

Amefahamisha kwamba hatua hiyo ni kuonesha utu na kuwathamini wananchi wenye shida mbali mbali  sambamba kujua hali zao na hivyo  kutafuta namna sahihi ya kuwasaidia kuzitatua.

Mhe. Othman leo ilikuwa ni siku ya tatu ya ziara yake hiyo ambapo tayari emetembelea majimbo yote ya Mkoa wa kusini na kaskzini  Unguja ambapo leo alitembelea majimbo ya wilaya za magharib  ‘A’ na ‘B’ na kesho atamaliza ziara hiyo kwa kuyatembelea majimbo ya wilaya ya mjini Unguja.

 

Mwisho

Imetolewa na ofisi ya Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha ACT Wazalendo leo Jumanne Februari 25, 2025.

Post a Comment

0 Comments