Joseph
Ngilisho, Arusha
WANAWAKE
wawili wanandugu wameuawa kinyama katika nyumba waliokuwa wakiishi na watu
wasiojulikana na miili yao
kukutwa baada ya siku tatu ikiwa imelaliana huku ikiwa imeharibika vibaya.
Kugundulika
kwa miili hiyo kumetokea jana majira ya saa 3:15 katika eneo la Daraja mbili manipsaa ya jiji ya Arusha baada ya majirani kuhisi harufu kali iliyokuwa
ikitokea ndani ya chumba walichokuwa wamepanga
katika nyumba inayomilikiwa na merehemu Samson Kivuyo.
Taarifa
zimeeleza kuwa majirani hao
walijikusanya na kutoa taarifa kwa uongozi wa eneo hilo ambao kwa pamoja
walikubaliana kutoa taarifa polisi
ambapo ,polisi walifika eneo la tukio na kuvunja mlango, ndipo walipokuta miili
ya marehemu hao ikiwa imeharibika vibaya.
Miiili
ya marehemu hao ilikutwa na majeraha sehemu mbalimbali za mwili, huku chumba
hicho kikiwa kimevurugika na baadhi ya vitu kuvunjika hali ambayo inaaminika
kwamba kabla ya mauaji hayo
kulikuwa
na mvutano mkubwa.
Akizungumza
na vyombo vya habari msimamizi wa nyumba hiyo,Fatina Mringo aliwataja marehemu
hao kuwa ni,Zainabu Iddy (Zai) mwenye umri wa miaka 19 na Zena Sadick Shengwatu
mwenye umri wa miaka 40 ambaye alikuwa mfanyabiashara wa nguo na mmiliki wa
chumba hicho.
Alieleza
kuwa siku ya Jumamosi marehemu hao walionekana majira ya mchana wakiwa nyumbani
na marehemu Zena alikabidhiwa fedha na wapangaji wenzake na kwenda kulipia bili ya umeme na baadae alirudi na kuendelea
na shughuli zake kama kawaida.
Hata
hivyo habari zimedai kwamba marehemu hao
kwa pamoja hawakuweza kuonekana tena hadi miili yao ilipokutwa chumbani ikiwa imeharibika vibaya
na kutoa harufu kali.
Hata
hivyo baadhi ya majirani wakielezea tukio hilo
wamebainisha kwamba marehemu hao mara nyingi walionekana kuwa na mahusiano ya kimapenzi
na wanaume tofauti na kwamba siku ya tukio Zena alionekana akichukuliwa na gari
dogo aina ya teksi huku gari jingine lilionekana likingia nyumbani kwake.
Majirani
hao wamedai kwamba marehemu hao ambao ni wakazi wa Lushoto mkoani Tanga
waliishi katika nyumba hiyo katika mazingira ya kutokuwa na waume.
Kamanda
wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo
na kueleza kwamba uchunguzi unaendelea na kwamba hadi sasa hakuna aliyekamatwa
kuhusiana na tukio hilo na miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospitali
ya mkoa Mount Meru kwa uchunguzi wa daktari.
No comments:
Post a Comment