VATICAN, Italia
KIONGOZI wa Kanisa Katoliki
Duniani, Papa Benedict wa XVI alionekana tena hadharani kwa mara ya mwisho jana
wakati alipowahutubia wafuasi wake katika ibada ya Jumapili.
Katika hotuba yake, Papa
Benedict alisema amejiuzulu kwa mapenzi ya Mungu na uamuzi wake huo kamwe hauna
maana kuwa amelitelekeza kanisa.
Akizungumza kwa hisia na
sauti nzito, Papa aliwambia maelfu kwa maelfu ya Wakiristu waliokusanyika
katika kanisa la St. Peter kuwa ataendelea kuliombea kanisa katika kipindi
chote kilichosalia cha maisha yake.
"Mwenyezi Mungu ndie
alieniambia nipumzike kutokana na afya yangu na kwa maslahi na utukufu wa
kanisa,” alisema huku akishangiriwa na umati mkubwa wa wafuasi wake ambao
walimtakia maisha marefu.
"Lakini hii haina maana
kwamba nimelitelekeza kanisa. Kawaida, kama Mwenyezi Mungu amenitaka nipumzike
ni lazima niheshimu kwa sababu naweza kuendelea kumtumikia kwa mapenzi yale
yale,” alisema.
Hotuba ya jana itakuwa ya
mwisho kwa Papa kabla ya Jumatano kufanya mkutano wake wa mwisho kama Papa na
baadae kukutana na Makadinali siku ya Alkhamis.
Nafasi ya upapa itakuwa wazi
kuanzia saa 2:00 asubuhi kwa saa za Italia siku ya Alkhamis.
Makadinali wataanza kukutana
siku ya Ijumaa kuandaa mkutano wa makadinali (conclave) ambao ni makhasusi kwa
kumchagua Papa mpya.
Kiongozi huyo (85) ambae
anaongoza Wakatoliki wapatao bilioni 1.2 duniani kote alisema anajiuzulu kwa
sababu afya yake imezorota na hana uwezo wa kutosha wa kulitumikia kanisa.
Aliwashuru waumini wa dini
ya kikiristu na kuwambia:”Siku zote tutaendelea kuwa pamoja”.
Polisi wa Vatican wanasema
zaidi ya watu 100,000 walimiminika katika makao makuu ya Papa kwenda
kumsikiliza kiongozi wao.
Benedict anakuwa Papa wa
kwanza kujiuzulu katika kipindi cha miaka 600 iliyopita.
No comments:
Post a Comment